Wanawake 100 katika orodha ya BBC mwaka 2022

Wanawake 100 wa BBC 2022: Ni nani aliye kwenye orodha mwaka huu?

Wanawake 100- BBC World Service

BBC imetoa orodha yake ya wanawake 100 wenye ushawishi duniani kwa mwaka 2022.

Miongoni mwao ni msanii maarufu wa muziki duniani Billie Eilish, Mke wa Rais wa Ukraine Olena Zelenska, waigizaji Priyanka Chopra Jonas na Selma Blair, 'tsarina wa pop wa Urusi' Alla Pugacheva, mpanda mlima wa Iran Elnaz Rekabi, mwanariadha aliyevunja rekodi ya kuruka mara tatu Yulimar Rojas, na mwandishi wa Ghana Nana Darkoa Sekyiamah.

Huu ni msimu wa kumi wa Wanawake 100 na, kwa hivyo, tunachukua fursa ya kutazama ni maendeleo gani yamepatikana katika miaka kumi iliyopita. Wakati kumekuwa na hatua kubwa za kupigania haki za wanawake - kutoka kwa idadi ya viongozi wa kike hadi vuguvugu la MeToo - kwa wanawake katika pembe nyingi za dunia bado inahisi kama kuna safari ndefu.

Orodha hiyo pia inaonesha jukumu la wanawake katika kitovu cha mizozo kote ulimwenguni mnamo 2022 - kutoka kwa waandamanaji wanaodai kwa ujasiri mabadiliko nchini Iran, hadi sura ya wanawake ya mzozo na upinzani nchini Ukraine na Urusi. Kwa mara ya kwanza mwaka huu, tumewaomba pia Wanawake 100 waliotangulia kuwateua wengine ambao waliona wanastahili nafasi katika orodha ya mwaka 2022.

Pata maelezo zaidi kuhusu wanawake 100 kwa kuchagua eneo unalotaka

Siasa & Elimu

Maeen Al-Obaidi

Maeen Al-Obaidi, Yemen

Mwanasheria

Wakati vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Yemen vikizidi kuongezeka mwaka huu, wakili Maeen Al-Obaidi anaendelea kuangazia ujenzi wa amani katika mji uliozingirwa wa Taiz. Amechukua jukumu la mpatanishi, kuwezesha kubadilishana wafungwa kati ya vikundi vinavyozozana. Ingawa hafanikiwi kila wakati kuwarejesha wapiganaji katika familia zao wakiwa hai, anajaribu kuhakikisha miili ya marehemu inarejeshwa.

Amejitolea kwa Umoja wa Wanawake wa Yemen, ambako aliwatetea wanawake waliofungwa. Pia alikuwa mwanamke wa kwanza kupandishwa cheo na kuwa kwenye Baraza la Wanasheria, akisimamia kamati ya haki za binadamu na uhuru.

Fatima Amiri

Fatima Amiri, Afghanistan

Mwanafunzi

Kijana wa Afghanistan, Fatima Amiri ni mmoja wa manusura wa shambulio la kujitoa muhanga katika kituo cha masomo mjini Kabul ambalo lilisababisha vifo vya zaidi ya watu 50, wengi wao wakiwa wanafunzi. Alipata majeraha mabaya, ikiwa ni pamoja na kupoteza jicho na uharibifu mkubwa wa taya na sikio.

Wakati akipona, alisomea mitihani yake ya kujiunga na chuo kikuu na kuifanya Oktoba, akipata zaidi ya 85%. Ndoto yake sasa ni kusoma sayansi ya kompyuta katika Chuo Kikuu cha Kabul na anasema kwamba kupoteza jicho lake katika shambulio hilo kumemfanya kuwa na nguvu na kujituma zaidi.

Nathalie Becquart

Nathalie Becquart, Vatican

Mtawa

Kuteuliwa kwake na Papa Francis kama msimamizi wa Sinodi ya Maaskofu kulimfanya kuwa mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huo. Katika jukumu hilo, yeye ni mmoja wa viongozi kadhaa wanaomshauri Papa kuhusu masuala muhimu kwa Kanisa Katoliki, pamoja na kuwa mwanamke pekee mwenye haki ya kupiga kura. Katibu Mkuu wa chombo hicho alisema mwaka 2021 kwamba uteuzi wake ulionesha kuwa "mlango umefunguliwa" kwa wanawake.

Hapo awali, mtawa wa Kifaransa wa Kutaniko la Xavières aliwahi kuwa mkurugenzi wa kwanza mwanamke wa Huduma ya Kitaifa ya Uinjilishaji wa Vijana na Wito nchini Ufaransa.

Kama papa Francis anavyosema, 'ni wajibu wa haki kupambana na ubaguzi na unyanyasaji wote' kwa wanawake... Kwa pamoja, tunahitaji kuunga mkono kwa njia yoyote ili kuhusisha wanawake zaidi katika nafasi za uongozi katika ngazi zote.

Nathalie Becquart

Taisia Bekbulatova

Taisia Bekbulatova, Urusi

Mwandishi wa habari

Mwandishi mashuhuri wa Urusi, Taisia Bekbulatova alianzisha chombo huru cha habari cha Holod mnamo 2019. Shirika hilo limeripoti sana juu ya vita nchini Ukraine, pamoja na kuchapisha hadithi kuhusu ukosefu wa usawa, vurugu, na haki za wanawake. Tovuti hiyo ilizuiwa nchini Urusi na mamlaka mwezi Aprili, wakati wa ukandamizaji dhidi ya vyombo huru vya habari.

Licha ya hayo, Bekbulatova na timu yake wameapa kuendelea na kazi yao, na wameshuhudia usomaji wao ukiongezeka. Bekbulatova, ambaye aliondoka Urusi mnamo 2021 baada ya kuitwa "wakala wa kigeni", amesafiri kwenda Ukraine mwenyewe kuripoti kuhusu vita kutoka mstari wa mbele.

Siamini katika maendeleo yasiyoepukika. Ustaarabu wa kisasa daima umeonekana kuwa dhaifu na rahisi kuharibu. Na haki za wanawake kwa kawaida huwa za kwanza kutoweka.

Taisia Bekbulatova

Kristina Berdynskykh

Kristina Berdynskykh, Ukraine

Mwandishi wa habari

Wakati wa vita nchini Ukraine, mwandishi wa habari aliyeshinda tuzo Kristina Berdynskykh amezunguka nchi yake, akiripoti kutoka mikoa ambayo ilikuwa chini ya mashambulizi ya Urusi. Baadhi ya kazi zake zimejikita hasa katika maelezo ya maisha ya kila siku katika jiji lenye migogoro.

Mzaliwa wa Kherson, Berdynskykh amefanya kazi kama mwandishi wa habari wa kisiasa kwa miaka 14 huko Kyiv, ikiwa ni pamoja na katika jarida la NV na miradi mbalimbali ya runinga na redio. Aliunda e-People, mradi wa vyombo vya habari vya kijamii kuhusu washiriki katika Mapinduzi ya Euromaidan ya Ukraine ambayo baadaye ikawa kitabu.

María Fernanda Castro Maya

María Fernanda Castro Maya, Mexico

Mwanaharakati wa ulemavu

Kama mwanamke mwenye ulemavu wa akili, Fernanda Castro anapigania wengine kama yeye kuweza kushiriki katika siasa. Yeye ni sehemu ya kundi la watetezi wa haki za walemavu, wanaoungwa mkono na Human Rights Watch, akivitaka vyama vyote vya kisiasa nchini Mexico kuwajumuisha watu wenye ulemavu wa akili na kujifunza katika sera zao.

Kazi yake inashughulikia upatikanaji wa lugha katika nyaraka zinazohusu maamuzi ya kisiasa, na kujumuishwa katika vyama vya siasa na matukio ya uchaguzi. Castro alikuwa sehemu ya ujumbe wa Mexico katika Umoja wa Mataifa ambao uliwasilisha ripoti kuhusu haki za walemavu, na ni mwakilishi wa mtandao wa kimataifa wa Inclusion International.

Chanel Contos

Chanel Contos, Australia

Mwanaharakati wa ridhaa ya ngono

Mwanzilishi wa vuguvugu lililopewa jina la 'Tufundishe Tukubali' ambalo linashawishi ridhaa kamili na elimu ya ujinsia, mnamo 2021 Chanel Contos alichapisha hadithi kwenye Instagram, akiwauliza wafuasi wake ikiwa wao au mtu wanayemjua alikuwa amenyanyaswa kingono shuleni. Ndani ya saa 24 zaidi ya watu 200 walikuwa wamejibu "ndiyo".

Alianzisha ombi la kutaka elimu ya idhini ya mapema nchini Australia. Kwa sababu ya kampeni yake, elimu ya ridhaa itakuwa lazima katika shule zote kuanzia chekechea hadi mwaka wa 10 kutoka 2023. Sasa anawaelimisha watu kuhusu kuondolewa kwa kondomu zisizo za kawaida, au kuiba, pamoja na kufanya kampeni ya kuharamisha kitendo hicho.

Eva Copa

Eva Copa, Bolivia

Mwanasiasa

Kiongozi wa zamani wa wanafunzi mwenye asili ya Aymara, Eva Copa anatikisa siasa nchini Bolivia. Baada ya kushindwa uteuzi wa chama chake kuwa meya wa El Alto, jiji la pili kwa ukubwa nchini humo, alisimama dhidi ya mgombea wao na kushinda kwa asilimia 69 ya kura. Hivi karibuni alitangaza mpango wa jiji hilo kwa wanawake, ambao utalenga kuimarisha haki za wanawake kupitia sera na uwekezaji.

Copa si mgeni katika siasa, baada ya kuhudumu kama seneta kati ya 2015 na 2020. Mgawanyiko wake na chama tawala unaonekana na wengi kama mabadiliko kuelekea mazingira tofauti ya kisiasa nchini Bolivia.

Tunahitaji viongozi zaidi wanawake: wanawake daima wanasimama wima, kamwe hawapigi magoti.

Eva Copa

Joy Ngozi Ezeilo

Joy Ngozi Ezeilo, Nigeria

Profesa wa sheria

Kama mkuu wa sheria katika Chuo Kikuu cha Nigeria na mwandishi maalum wa zamani wa Umoja wa Mataifa juu ya usafirishaji haramu wa watu, Joy Ezeilo ni mamlaka inayoongoza katika uwanja wa haki za binadamu za kimataifa.

Yeye ni mkurugenzi mwanzilishi wa Women Aid Collective (WACOL), ambayo katika miaka 25 iliyopita imetoa msaada wa kisheria na makazi bure kwa wanawake 60,000 walio katika mazingira magumu nchini Nigeria. Pia alianzisha Kituo cha Rufaa ya Unyanyasaji wa Kijinsia cha Tamar, ili kutoa majibu ya haraka kwa waathirika na manusura wa unyanyasaji.

Chimamanda Ngozi Adichie

Aliteuliwa na mshindi wa 2021, mwandishi Chimamanda Ngozi Adichie

"Profesa Ezeilo amegusa maisha ya watu wengi kupitia utoaji wa msaada wa kisheria bure kwa maskini, hasa kwa wanawake na wasichana ambao haki zao za binadamu zimekiukwa.

Ibijoke Faborode

Ibijoke Faborode, Nigeria

Mwanzilishi mwenza wa ElectHER

Kupitia electHER, Ibijoke Faborode anafanya harakati za kisiasa za wanawake nchini Nigeria. Shirika lake linafanya kazi ya kuziba mapengo ya ukosefu wa usawa katika uwakilishi wa kisiasa na limeshirikisha zaidi ya wanawake 2,000 katika siasa kote Barani Afrika. Pamoja na kampeni za #Agender35, shirika lake linaunga mkono moja kwa moja wanawake 35 wanaowania nafasi za mitaa au shirikisho katika uchaguzi mkuu wa 2023, wakitoa rasilimali watu na fedha.

Pia ameanzisha programu ya kwanza ya simu ya Kiafrika ya wanawake ya uchambuzi wa data za uchaguzi. Faborode kwa sasa anahudumu katika Baraza la Uongozi la The Democracy and Culture Foundation, ambalo linabainisha njia mpya za kuboresha michakato ya kidemokrasia.

Erika Hilton

Erika Hilton, Brazil

Mwanasiasa

Mwanamke wa kwanza mweusi mwenye jinsia mbili kuwahi kuchaguliwa katika bunge la kitaifa la Brazil. Erika Hilton ni mwanaharakati anayefanya kampeni dhidi ya ubaguzi wa rangi, na kwaajili ya haki za watu wa mapenzi ya jinsia moja.

Akiwa kijana, alifukuzwa kutoka nyumba ya familia ya kihafidhina na kuishi mitaani, kabla ya kwenda chuo kikuu. Akiwa na historia katika siasa za wanafunzi, Hilton alihamia São Paulo na kujiunga na chama cha mrengo wa kushoto cha PSOL. Mwaka 2020 alichaguliwa katika baraza la jiji na akaendelea kuandika sheria iliyoanzisha mfuko wa manispaa dhidi ya njaa katika mji mkubwa wa Brazil.

Mapambano yetu ni kufikia haki sawa, mishahara sawa na mwisho wa unyanyasaji wa kijinsia, iwe sisi ni weusi, Kilatini, weupe, maskini, matajiri, cis au waliobadili jinsia.

Erika Hilton

Park Ji-hyun

Park Ji-hyun, Korea Kusini

Mwanamageuzi wa kisiasa

Akiwa mwanafunzi wa chuo kikuu, Park Ji-hyun bila kujulikana alisaidia kubwa zaidi la uhalifu wa kingono mtandaoni nchini Korea Kusini, maarufu kama Nth rooms. Mwaka huu alijitokeza hadharani na uzoefu wake na kuingia katika siasa, akiwafikia wapiga kura vijana.

Chama cha Democratic kiliposhindwa katika kinyang'anyiro cha urais, walimtaja kiongozi mwenzake wa mpito. Pia alikuwa katika kamati ya wanawake, ambayo ililenga kukabiliana na uhalifu wa kingono kidijitali. Mwezi Juni, chama hicho kilikabiliwa na hasara zaidi na akajiuzulu. Ingawa huenda asiwe na jukumu rasmi kwa sasa, bado amejitolea kushinikiza usawa wa kijinsia katika siasa.

Duniani kote, uhalifu wa kingono kidigitali unatishia haki za wanawake na tunahitaji kutatua tatizo hili kwa mshikamano.

Park Ji-hyun

Zahra Joya

Zahra Joya, Afghanistan

Mwandishi wa habari

Kwa miaka sita chini ya utawala wa Taliban, Zahra Joya akawa 'Mohammad' na kuvaa kama mvulana kuhudhuria shule. Wakati vikosi vinavyoongozwa na Marekani vilipowaangusha Taliban mwaka 2001 alirudi shuleni kama Zahra. Alianza kufanya kazi kama mwandishi wa habari mwaka 2011 na mara nyingi alikuwa mwandishi pekee wa katika chumba cha habari.

Yeye ndiye mwanzilishi wa Rukhshana Media, shirika pekee la habari za nchini Afghanistan, lililopewa jina la kijana wa miaka 19 ambaye alipigwa mawe hadi kufa na Taliban. Joya alihamishwa kutoka Afghanistan mnamo 2021 na sasa anaendesha Rukhshana Media kutoka uhamishoni nchini Uingereza. Alishinda Tuzo ya Gates Foundation ya 2022 Changemaker.

Ninaamini katika nguvu ya maneno na lazima tuzungumzie dhuluma dhidi ya wanawake.

Zahra Joya

Ursula von der Leyen

Ursula von der Leyen, Ujerumani

Rais wa Tume ya Ulaya

Rais wa kwanza mwanamke wa Tume ya Umoja wa Ulaya, Ursula von der Leyen ni mwanasiasa wa Ujerumani. Alihudumu katika baraza la mawaziri la Angela Merkel na alikuwa waziri wa kwanza mwanamke wa ulinzi kuwahi kuteuliwa nchini Ujerumani.

Alizaliwa Brussels, alisomea uchumi na dawa kabla ya kuingia katika siasa. Alichukua kazi ya juu ya EU mnamo 2019, na tangu wakati huo ameongoza umoja huo kupitia Brexit, janga la Covid-19, na vita nchini Ukraine. Alikuwa msukumo mkubwa kwa sheria ya EU inayohitaji usawa wa kijinsia kwenye bodi za kampuni ambazo zilipitishwa mwaka huu.

Sanna Marin

Aliteuliwa na mshindi wa 2020, Waziri Mkuu wa Finland Sanna Marin

"Wakati Ulaya ikikabiliwa na mgogoro mmoja baada ya mwingine, Ursula von der Leyen ameonesha uamuzi wa ajabu katika kusaidia Umoja wa Ulaya kupitia changamoto hizi kwa pamoja. Uongozi wake umekuwa na mashiko. Nyakati ni ngumu, lakini yeye ameendelea kuwa na nguvu zaidi."

Naomi Long

Naomi Long, Ireland Kaskazini

Mwanasiasa

Waziri wa zamani wa sheria Naomi Long alileta sheria ya kukabiliana na makosa kadhaa mapya ya kingono kaskazini mwa Ireland mwaka huu, ikiwa ni pamoja na kuvua nguo, kuangaza mtandaoni na kukomesha utetezi wa 'ngono mbaya'. Baada ya kupokea vitisho vya kuuawa, Long pia ametaka kuhamasisha umma kuhusu unyanyasaji wa wanasiasa wanawake.

Mhandisi wa kiraia kwa taaluma, alijiunga na chama cha Alliance mwaka 1995. Baada ya kuhudumu kama Meya wa Belfast, alikuwa mbunge wa kwanza wa Muungano kuchaguliwa westminster mnamo 2010, akimtoa waziri wa zamani wa kwanza Peter Robinson kutoka kiti cha Westminster alichokuwa ameshikilia kwa zaidi ya miaka 30.

Tunahitaji kukabiliana na mitazamo inayojenga mazingira ambayo unyanyasaji bado ni wa kawaida. Hiyo inamaanisha sisi sote moja kwa moja na mara kwa mara tunapinga utamaduni wa mfumo dume, ujinsia, na upotoshaji.

Naomi Long

Ayesha Malik

Ayesha Malik, Pakistan

Hakimu

Akiwa ameteuliwa mwaka huu kama jaji wa kwanza mwanamke wa Mahakama Kuu ya Pakistan, Jaji Ayesha A. Malik ameandika hukumu zinazolinda haki za wanawake. Hii ni pamoja na hukumu yake ya kihistoria ambayo ilipiga marufuku kile kinachoitwa kipimo cha vidole viwili vya waathiriwa wa ubakaji. 'Vipimo hivi vya ubikira' vilikuwa vikifanywa wakati wa uchunguzi wa kesi za unyanyasaji wa kijinsia hadi vilipopigwa marufuku mwaka 2021.

Pamoja na jukumu lake katika Mahakama ya Juu, Malik pia anaendesha mafunzo kwa majaji kote ulimwenguni na amezindua mikutano kwa majaji wanawake nchini Pakistan, akihimiza mjadala kuhusu mtazamo wa kijinsia katika mfumo wa haki.

Wanawake lazima wajenge hadithi mpya - ambayo inajumuisha mtazamo wao, inatoa uzoefu wao, na inajumuisha hadithi zao.

Ayesha Malik

Zara Mohammadi

Zara Mohammadi, Iran

Muelimishaji

Kama mmoja wa waanzilishi wa Chama cha Kijamii na Utamaduni cha Nojin, Zara Mohammadi amejitolea zaidi ya muongo mmoja kufundisha lugha ya Kikurdi katika mji wake wa Sanandaj.

Katiba ya Iran inasema kuwa matumizi ya lugha za kikanda na kikabila yanaruhusiwa kwa uhuru katika mazingira ya elimu, lakini wanasheria na wanaharakati wanasema hilo halipo kwa vitendo, hivyo watoto hawawezi kujifunza lugha yao mama shuleni. Serikali ya Iran ilimshutumu Mohammadi kwa "kuunda makundi na jamii kwa lengo la kuvuruga usalama wa taifa" na alihukumiwa kifungo cha miaka mitano jela. Amekuwa gerezani tangu Januari 2022.

Mia Mottley

Mia Mottley, Barbados

Waziri Mkuu

Kama waziri mkuu wa kwanza mwanamke wa Barbados, Mia Mottley alishinda muhula wa pili madarakani baada ya ushindi wa kishindo, mwezi Januari. Ameongoza chama cha Barbados Labour tangu 2008. Aliongoza kisiwa cha Caribbean wakati ikikata uhusiano na familia ya kifalme ya Uingereza, akimwondoa mfalme kama mkuu wa nchi na kuwa jamhuri mpya zaidi duniani.

Mottley anajulikana kwa kukasirishwa na mabadiliko ya tabia nchi. Katika mkutano wa COP27 aliyakosoa mataifa tajiri kwa kushindwa kukabiliana na mzozo wa hali ya hewa, akionya kuwa huenda kukawa na wakimbizi bilioni moja wanaotokana na mabadiliko ya tabis nchi ifikapo mwaka 2050 iwapo hatua hazitachukuliwa.

Sepideh Qoliyan

Sepideh Qoliyan, Iran

Mwanaharakati wa kisiasa

Mwanafunzi wa sheria Sepideh Qoliyan alihukumiwa kifungo cha miaka mitano jela kwa kuunga mkono haki za wafanyakazi katika jimbo la Khuzestan, kusini magharibi mwa Iran. Ametumia miaka minne iliyopita katika magereza manne tofauti ya Iran, ikiwa ni pamoja na Evin, eneo la msingi la makazi ya wafungwa wa kisiasa.

Hata kutoka gerezani, anaendelea na kazi yake, baada ya kutuma mkanda wa sauti unaoelezea ''vitendo vya kinyama'' aliyokumbana nayo. Pia anafanya kazi kama sauti kwa wafungwa wa na, akiwa kwa dhamana, aliandika kitabu kuhusu "mateso" na "dhuluma" ambayo wanawake hupitia katika magereza ya Iran.

Roza Salih

Roza Salih, Uskoti

Mwanasiasa

Mnamo Mei 2022, Roza Salih alikuwa mkimbizi wa kwanza kuchaguliwa katika Baraza la Jiji la Glasgow, baada ya kuwasili Scotland kama msichana mdogo wakati familia yake ilipolazimika kutoroka Iraq. Sasa diwani wa SNP wa kata ya Greater Pollok, Salih amekuwa akifanya kampeni ya haki za wakimbizi tangu akiwa kijana na yeye na marafiki zake wa shule waliungana kupinga kukamatwa kwa rafiki yake.

Kampeni yao, Glasgow Girls, ilivutia hisia za kitaifa kwa matibabu ya waomba hifadhi. Salih ameendelea kushirikiana wa Scotland na Kurdistan, akitembelea mikoa ya Kikurdi nchini Uturuki kama mwanaharakati wa haki za binadamu.

Simone Tebet

Simone Tebet, Brazil

Mbunge wa Seneti ya Shirikisho la Brazil

Akionekana na wengi kama kielelezo cha kupinga ubaguzi nchini humo, Seneta wa Brazil wa mrengo wa kati Simone Tebet alimaliza wa tatu katika kinyang'anyiro cha urais mwaka huu. Alichaguliwa mwakilishi wa jimbo mwaka 2002 na meya wa mji wake Três Lagoas mwaka 2004 na 2008. Mwaka 2014, alichaguliwa kuwa mbunge wa Seneti kwa zaidi ya asilimia 52 ya kura halali.

Alikuwa mwanamke wa kwanza kuwa mwenyekiti wa Kamati ya Katiba na Haki ya Seneti, inayochukuliwa kuwa jopo muhimu zaidi la bunge hilo. Profesa wa sheria kwa zaidi ya muongo mmoja, Tebet pia alikuwa mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Kupambana na Unyanyasaji dhidi ya Wanawake.

Kila mtu anapaswa kujua kuwa siku zijazo ni za mwanamke, na nafasi ya mwanamke ni popote anapotaka.

Simone Tebet

Kisanet Tedros

Kisanet Tedros, Eritrea

Mjasiriamali wa elimu

Beles Bubu ni chaneli ya YouTube ambayo inafundisha watoto wa Eritrea lugha na utamaduni wao, iliyoanzishwa na muundaji wa maudhui na mjasiriamali Kisanet Tedros. Alizaliwa na kukulia Ethiopia, tangu akiwa mdogo alithamini umuhimu wa kuelewa lugha ili kujisikia kushikamana na asili ya mtu.

Timu yake ya uzalishaji huleta pamoja wasanii wa sauti na digitali kutoka Eritrea, Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ili kuunda maudhui ya kidigitali. Video hizo zinafikiwa na wazazi wanaozungumza Tigrinya na watoto wao kutoka Eritrea na Ethiopia. Tedros pia aliandaa tamasha la kwanza la watoto la Beles Bubu kwa wakimbizi mjini Kampala, Uganda.

Cheng Yen

Cheng Yen, Taiwan

Mhisani wa Kibudha

Dharma Mwalimu Cheng Yen anaonekana kama mmoja wa watu wenye ushawishi mkubwa katika maendeleo ya Ubuddha wa kisasa wa Taiwan. Mwanzilishi wa wakfu wa kibinadamu wa Tzu Chi, wakati mwingine hujulikana kama 'Mama Teresa wa Asia'.

Alianzisha shirika hilo mwaka 1966, huku mama wa nyumbani 30 pekee wakiokoa pesa za kusaidia familia zenye uhitaji. Tangu wakati huo imekua na mamilioni ya wafuasi ulimwenguni, kutoa misaada ya kimataifa na misaada ya matibabu, na kuendesha shule na hospitali. Sasa mwishoni mwa miaka ya 80, wafuasi wake wanaendelea na kampeni zao za uhisani na hivi karibuni walitoa misaada ya kifedha na vifaa kwa wakimbizi kutoka Ukraine iliyokumbwa na vita.

Nazanin Zaghari-Ratcliffe

Nazanin Zaghari-Ratcliffe, Uingereza/Iran

Mfanyakazi wa hisani

"Dunia inapaswa kuungana kuhakikisha kuwa hakuna mtu anayeshikiliwa ama mateka au gerezani kwa jambo ambalo hawajalifanya" yalikuwa maneno ya Uingereza na Iran Nazanin Zaghari-Ratcliffe baada ya kuachiliwa huru na mamlaka ya Iran mwezi Machi, baada ya kampeni ya muda mrefu ya mumewe Richard kushinikiza serikali ya Uingereza kutaka aachiliwe huru na kutatua mzozo wa kihistoria wa madeni na Iran.

Zaghari-Ratcliffe alikamatwa kiholela nchini Iran wakati akiwa likizoni na binti yake mwaka 2016, na hatimaye kama mwanadiplomasia alishikiliwa mateka na mamlaka ya Iran kuweka shinikizo kwa serikali ya Uingereza. Alizuiliwa kwa miaka sita, awali alihukumiwa na Mahakama ya Mapinduzi kwa kujaribu kuupindua utawala wa Iran. Wakati hukumu yake ya kwanza ilipohitimishwa mwaka 2021, alipewa hukumu ya pili, na kuzuiliwa nchini Iran hadi makubaliano ya kidiplomasia yalipofikiwa. Zaghari-Ratcliffe amekanusha vikali madai yote, na anaandika kumbukumbu na mumewe.

Olena Zelenska

Olena Zelenska, Ukraine

Mke wa rais

Mwandishi wa televisheni aliyefanikiwa alikuwa akifanya kazi nyuma ya pazia, Olena Zelenska aliingizwa kwenye jukwaa la dunia wakati mumewe, Volodymyr Zelenskyy, alipokuwa rais wa Ukraine mnamo 2019. Kama Mke wa Rais amefanya kazi kuboresha haki za wanawake na kukuza utamaduni wa Kiukraine

Baada ya uvamizi wa Urusi, alitumia jukwaa lake kuangazia mateso ya watu wa Ukraine, na kuwa mke wa kwanza wa rais wa kigeni kuhutubia Bunge la Marekani. Sasa analenga kutoa msaada wa afya ya akili kwa watoto na familia zilizoathiriwa na vita.

Wanawake wamechukua majukumu mengi zaidi kuliko wakati wa amani... Mwanamke aliyepitia vita hii kamwe hawezi kurudi nyuma. Na nina uhakika kwamba imani yetu ya ndani itaongezeka.

Olena Zelenska

Utamaduni & Michezo

Dima Aktaa

Dima Aktaa, Syria

Mkiambiaji

Mwaka 2012, nyumba ya Dima Aktaa nchini Syria ilipigwa mabomu. Alipoteza mguu wake na uwezo wa kufanya moja ya vitu anavyovipenda - kukimbia. Takriban 28% ya Wasyria wana ulemavu, karibu mara mbili ya wastani wa kimataifa, kulingana na takwimu za Umoja wa Mataifa. Miaka kumi baadaye, Aktaa yuko Uingereza, akifanya mazoezi ya kushindana katika Michezo ya Olimpiki ya Walemavu ya 2024.

Baada ya kuchangisha pesa kwa ajili ya wakimbizi wakati wa janga la corona, alitambuliwa kama mwanachama wa kikosi mbadala cha soka cha Uingereza, Simbahearts. Hadithi yake hivi karibuni iliangaziwa katika video ya muziki ya nyota wa muziki wa Anne-Marie Beautiful, na anaendelea kuhamasisha watu wenye ulemavu.

Zar Amir-Ebrahimi

Zar Amir-Ebrahimi, Iran

Muigizaji

Mwaka huu, mwigizaji aliyeshinda tuzo na mtengenezaji wa filamu Zar Amir-Ebrahimi alikuwa raia wa kwanza wa Iran kushinda tuzo ya muigizaji bora wa huko Cannes kwa uigizaji wake huko Holy Spider, filamu iliyotokana na hadithi ya kweli ya muuaji wa mfululizo ambaye aliwalenga wafanyabiashara ya ngono.

Amir-Ebrahimi alilazimika kuondoka Iran ili kuepuka mateso na kushtakiwa, baada ya video yake ya faragha kuvujishwa na kufanyiwa kampeni kali kuhusu maisha yake ya mapenzi. Mnamo 2008 alihamia Paris, alianzisha kampuni yake ya uzalishaji Alambic Production, na ameendelea kujenga kazi ya kuvutia mbele na nyuma ya kamera.

Selma Blair

Selma Blair, Marekani

Muigizaji

Known for her roles in pop-culture classics Cruel Intentions, Legally Blonde and the Hellboy franchise, Selma Blair is an American film and television actress.

Aligundulika kuwa na maradhi ya ubongo na uti wa mgongo mwaka 2018 na amesifiwa kwa kuhamasisha jamii kuhusu hali hiyo, akizungumza kwa uwazi kuhusu safari yake ya kiafya na changamoto anazokumbana nazo. Mwaka huu, alitoa kumbukumbu yake 'Mean Baby', na kushirikiana na chapa, kwa lengo la kutengeneza vipodozi vya ergonomic ambavyo ni rahisi kutumia kwa kila mtu.

Mimi ni mwanamke ambaye nimekuwa na wakati mgumu, ambaye anaweza kuhukumiwa kwa mambo mengi na inaweza kunivunjwa nguvu zangu kwa urahisi sana, lakini imekuwa kupitia msaada wa wanawake wengine ambao niko hapa.

Selma Blair

Ona Carbonell

Ona Carbonell, Hispania

Muogeleaji

Muogeleaji wa Hispania Ona Carbonell anafanya kampeni za kurekebisha mtazamo wa kuwa mama na mwanariadha msomi. Mwanamichezo mara tatu, amekusanya zaidi ya medali 30, zikiwemo fedha za Olimpiki na shaba.

Mnamo 2020, alijifungua mtoto wake wa kwanza na kuanza mazoezi ya kuweza kufika Olimpiki ya Tokyo. Alielezea masikitiko yake juu ya sheria ambazo zilimaanisha kuwa hangeweza kumnyonyesha mwanawe katika hafla hiyo. Mwaka huu amekuwa mama kwa mara ya pili. Alisimulia hadithi yake katika makala ya kuwaonesha wanariadha wengine wa kwamba uzazi unaweza kuendana na michezo.

Sarah Chan

Sarah Chan, Sudani Kusini

Skauti wa NBA

Mchezaji wa zamani wa mpira wa kikapu Sarah Chan sasa anawashauri vijana na kuwafundisha mchezo huo nchini Sudan Kusini na Kenya. Yeye pia ni meneja wa kwanza wa wa skauti barani Afrika kwa timu ya mpira wa kikapu ya NBA ya Toronto Raptors.

Baada ya kukimbia vita huko Khartoum, Sudan, yeye na familia yake walihamia Kenya, ambako kazi ya mpira wa kikapu ya Chan ilianza. Alipata udhamini wa mpira wa kikapu katika Chuo Kikuu cha Umoja huko Jackson, Tennessee, na alicheza barani Afrika na Ulaya. Chan alianzisha Home At Home/Apediet Foundation, shirika lisilo la kiserikali linalopambana na ndoa za utotoni, kutetea elimu, na hutumia michezo kuelimisha vijana.

Wewe ndiye yule unayejiamini mwenyewe, hivyo amini katika siku zijazo zinazostahili ndoto na matarajio yako yote.

Sarah Chan

Priyanka Chopra Jonas

Priyanka Chopra Jonas, India

Muigizaji na mtayarishaji

Akiwa na filamu zaidi ya 60 kwa jina lake, Priyanka Chopra Jonas ni mmoja wa waigizaji wakubwa wa filamu wa Bollywood. Baada ya filamu yake ya kwanza mnamo 2002, mafanikio ya Miss World wa zamani huko Hollywood yalikuja wakati alipoweka historia kama muigizaji wa kwanza wa Asia Kusini kuongoza mfululizo wa maigizo ya mtandao wa Amerika (Quantico, 2015).

Sifa zake za uigizaji wa Hollywood ni pamoja na Isn't It Romantic na The Matrix Resurrections. Ameanzisha kampuni yake ya uzalishaji, akitengeneza filamu nchini India. Chopra pia ni Balozi wa Nia Njema wa Unicef, anayepigania haki za watoto na elimu kwa wasichana.

Harakati ya MeToo na sauti zinazofuata za wanawake kuja pamoja, kulindana, na kusimama na kila mmoja - kuna kitu chenye nguvu sana katika umoja.

Priyanka Chopra Jonas

Billie Eilish

Billie Eilish, Marekani

Mwimbaji-mwandishi

Nyota aliyeshinda tuzo ya Grammy na kuvunja rekodi Billie Eilish anajulikana kwa kupeleka muziki wake nje ya mipaka - kutokana na wimbo wake wa Your Power, ambao unawaita wanyanyasaji wanaowanyonya wasichana wenye umri mdogo, mpaka kibao chake cha All The Good Girls Go To Hell, wimbo unaohusu mabadiliko ya tabia nchi

Aliweka historia mwaka huu kwa kuwa kichwa cha habari akiwa na umri mdogo zaidi wa Glastonbury kuwahi kutokea, akitumia mpango wake wa kupinga uamuzi wa Mahakama Kuu ya Marekani wa kukomesha haki ya kikatiba ya utoaji mimba. Amezungumza wazi kuhusu picha ya mwili, vipindi vyake vya msongo wa mawazo na kuishi na ugonjwa wa Tourette.

Naogopa sana muda tulionao sasa hivi. Wanawake wakiwa kileleni. Kulikuwa na kipindi maalum ambapo nilikuwa katika shimo hili la kukosa matumaini kwa sababu hakukuwa na wasichana kama mimi kuchukuliwa kwa uzito.

Billie Eilish

Ons Jabeur

Ons Jabeur, Tunisia

Mcheza tenisi

Baada ya kuweka historia kwenye Mashindano ya Wimbledon ya 2022, nyota wa tenisi wa Tunisia Ons Jabeur alikuwa mwanamke wa kwanza wa Kiarabu au Kiafrika kufika fainali ya Grand Slam katika michuano ya Wazi. Miezi michache baadaye, alifika fainali ya US Open.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28, ambaye alianza kucheza tenisi akiwa na umri wa miaka mitatu tu, alifanikiwa kushika namba mbili katika orodha ya Chama cha Tenisi cha Wanawake (WTA) - nafasi ya juu zaidi kuwahi kushikiliwa na Mwafrika au Mwarabu, iwe mwanaume au mwanamke. Jabeur ameshinda mataji matatu ya pekee, na amesifiwa kwa kuhamasisha kizazi kipya cha wachezaji.

Sneha Jawale

Sneha Jawale, Sneha Jawale

Mfanyakazi wa kijamii

Wakati wazazi wake hawakuweza kutimiza mahitaji ya mahari zaidi mnamo Desemba 2000, mume wa Sneha Jawale alimchoma moto kwa mafuta ya taa. Familia hiyo haikuwasilisha malalamiko polisi. Baada ya mumewe kuondoka na mtoto wao, aliamua kujenga upya maisha yake, kama msomaji wa kadi ya tarot na mwandishi wa mswada - kazi ambazo watu hawakulazimika kuona uso wake.

Jawale, now a social worker, was asked to star in a theatre play, Nirbhaya, named after the 2012 Delhi gang-rape victim and based on the experiences of survivors of violence. Performing to audiences around the world helped her overcome her fears.

Katika kipindi cha miaka 10 iliyopita, mitazamo ya jamii juu ya manusura wa kuungua na tindikali imebadilika. Sijichukulii chini ya Miss World au Miss Universe. Nasema mimi ni mrembo.

Sneha Jawale

Reema Juffali

Reema Juffali, Saudi Arabia

Dereva wa gari za mashindano

Mnamo 2018, Reema Juffali aliweka historia kwa kuwa dereva wa kwanza wa mbio za wa Saudi Arabia.Mwaka huu, alianzisha timu yake mwenyewe, Theeba Motorsport, kushindana katika GT Open ya Kimataifa na kuboresha ufikiaji wa Saudi Arabia na ushiriki katika mbio za magari. Kupitia timu hiyo, dereva mtaalamu anatengeneza fursa na programu mbalimbali za elimu ili kuboresha utofauti katika michezo.

Mfano wa kuigwa kwa madereva wengine wa kike wa mbio kote ulimwenguni, Juffali anatarajia kuwa wa kwanza - akishindana mbio za kifahari za Le Mans za saa 24 na Theeba Motorsport.

Mitazamo hasi mingi inabaki kwa wanawake katika jamii. Msaada unahitajika kutoka nyumbani, na pia kutoka kwa jamii, ili mabadiliko ya maana na ya kudumu yatokee.

Reema Juffali

Kadri Keung

Kadri Keung, Hong Kong

Mbunifu wa mavazi

Kubuni mavazi ya kupendeza kwa wazee na kwa miili tofauti ni shauku kwa Kadri Keung. Alianza chapa ya mitindo ya kubadilisha RHYS na mama yake Ophelia Keung mnamo 2018, akiongozwa na kumtunza bibi yake Kadri na kutambua kuwa mavazi kwa wazee mara nyingi hayana mtindo na utendaji.

Kama mhitimu wa ubunifu wa mavazi, Keung anachanganya ujuzi wake na mahitaji ya mteja, iwe ni kufunga velcro au mfuko wa kushikilia catheter. Chapa yake iliajiri na kutoa mafunzo kwa wanawake 90 wasio na uwezo, wakiwemo baadhi ya watu wenye ulemavu. Mnamo 2022, Keung ilianzisha Boundless, chapa inayojumuisha kukuza vitu vya kazi vya mitindo.

Mie Kyung (Miky) Lee

Mie Kyung (Miky) Lee, Korea Kusini

Mtayarishaji

Kama msaidizi mwenye shauku ya sanaa, Miky Lee anaongoza wimbi la kitamaduni la Kikorea. Yeye ni chachu ya mafanikio ya K-pop ulimwenguni na mbunifu wa tamasha la muziki KCON. Yeye pia ni mtayarishaji mtendaji wa Parasite, filamu ya kwanza ya lugha ya kigeni kushinda tuzo ya Oscar kwenye kipengele cha picha bora.

Lee ni Makamu Mwenyekiti wa kampuni ya burudani ya Korea Kusini CJ ENM - studio yenye nguvu ya filamu na televisheni, mwendeshaji wa kebo na kampuni ya uzalishaji wa muziki.

Rebel Wilson

Aliteuliwa na mshindi wa 2021, mwigizaji Rebel Wilson

"Yeye ni NGUVU YA MSICHANA, na mfano wa kuigwa kwangu. Amewakilisha na kukuza utamaduni wake kwa ulimwengu''

Laura McAllister

Laura McAllister, Wales

Profesa na Mcheza kandanda wa zamani

Nahodha wa zamani wa timu ya soka ya wanawake ya Wales, Laura McAllister ameshikilia majukumu kadhaa ya juu katika utawala wa michezo. Kwa sasa ni Naibu Mwenyekiti wa Kamati ya Soka ya Wanawake ya Uefa na alisimama kwenye uchaguzi kama mwakilishi wa Uefa kwenye Baraza la Fifa mnamo Aprili 2021. Yeye ni mkurugenzi wa bodi katika Chama cha Soka cha Wales Trust.

Hivi sasa ni profesa katika Chuo Kikuu cha Cardiff, McAllister ni mtaalamu wa siasa za Wales. Mwaka huu, alichaguliwa na Wales kama balozi wa michezo wa LGBTQ + kuhudhuria Kombe la Dunia nchini Qatar. Alitakiwa kuondoa kofia yake ambayo ilionesha kuiunga mkono jamii ya LGBTQ+ alipokuwa akiingia uwanjani.

Milli

Milli, Thailand

Msanii wa Rap

Msanii na mtunzi wa nyimbo Danupha Khanatheerakul, anayejulikana zaidi kwa jina lake la jukwaani Milli, anatumia mashairi yenye utata kushughulikia masuala kama vile viwango vya urembo visivyo halisi na idhini ya ngono. Anaimba kwa lugha na lahaja nyingi, pia akijumuisha misimu kutoka kwa jamii ya watu waliobadili jinsia nchini Thailand. Hivi karibuni alitangaza albamu yake ya kwanza inayoitwa BABB BUM BUM.

Alifanya ushawishi katika tamasha la Coachella mwaka huu kwa kupinga mila potofu za Thailand na serikali, pamoja na kula wali wa maembe kwenye jukwaa, kitinda mlo (dessert) cha jadi cha Thailand. Mwaka jana alikabiliwa na mashtaka ya kashfa kwa kukosoa hatua ya serikali ya Thailand ya kukabiliana na Covid-19. Matokeo yake, hashtag #SaveMilli ilikuwa maarufu.

Rita Moreno

Rita Moreno, Puerto Rico/Marekani

Muigizaji

Wasanii wachache sana hupata hadhi ya EGOT - neno la mafanikio makubwa ya kushinda Tuzo ya Emmy, Grammy, Oscar, na Tony - lakini Rita Moreno ni mmoja wao. Muigizaji huyo wa Puerto Rico, mwimbaji na mcheza densi alitoa wimbo wa kwanza akiwa na umri wa miaka 13 na amekuwa na kazi nzuri kwa miongo saba.

Alionekana kwenye filamu ya Singin' in the Rain na The King and I, lakini alikuwa Anita katika Hadithi ya awali ya Upande wa Magharibi ambayo ilimfanya kuwa Mlatino wa kwanza kuwahi kushinda tuzo ya Oscar. Steven Spielberg mshiriki mpya kabisa aliyoandikwa katika marekebisho yake yaliyosifiwa hasa kwa Moreno, sasa katika miaka yake ya 90.

Salima Rhadia Mukansanga

Salima Rhadia Mukansanga, Rwanda

Mwamuzi

Katika wakati wa kihistoria kwa soka ya kimataifa, Salima Rhadia Mukansanga alichaguliwa na Fifa kama mmoja wa waamuzi watatu wa kwanza wa wanawake kushiriki Kombe la Dunia la wanaume, nchini Qatar 2022 - ikiwa ni mara ya kwanza kwa michuano hiyo kuwa na wanawake katika nafasi hiyo katika miaka yake 92.

Januari mwaka jana, alikuwa mwanamke wa kwanza kurejelea mechi katika fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wanaume, na pia alijitosa kwenye Michezo ya Olimpiki jijini Tokyo. Tayari ameongoza michezo katika kiwango cha juu zaidi katika soka ya kimataifa ya wanawake. Kabla ya kufanya kazi katika michezo, alipata mafunzo ya ukunga.

Alla Pugacheva

Alla Pugacheva, Urusi

Mwanamuziki

Msanii na mtunzi Alla Pugacheva ameuza zaidi ya rekodi milioni 250. Akiwa na maonesho ya nyimbo zaidi ya 500 na albamu 100, 'tsarina ya pop ya Kirusi' ni ikoni ya kitamaduni, inayojulikana kwa sauti yake ya wazi ya mezzo-soprano, ingawa sasa amestaafu kutumbuiza.

Amekuwa akiheshimiwa mara kwa mara na Urusi kwa muziki wake, lakini Pugacheva amezungumza dhidi ya serikali mara kadhaa. Hivi karibuni alichapisha ujumbe kwa wafuasi wake milioni 3.6 kwenye Instagram akilaani vita nchini Ukraine, wengine walimpa sifa wengine walimpa shutuma za uhaini.

Dunia imeshuhudia mafanikio makubwa katika kupigania upatikanaji wa elimu kwa wanawake na uhuru wa kifedha. Hata hivyo, unyanyasaji wa nyumbani bado ni tatizo kubwa katika nchi nyingi.

Alla Pugacheva

Elnaz Rekabi

Elnaz Rekabi, Iran

Mpandaji

Katika mashindano ya Asia yaliyofanyika Korea Kusini mwezi Oktoba, mpandaji wa Iran Elnaz Rekabi alishindana bila hijabu, huku kukiwa na maandamano dhidi ya hijabu ya lazima nchini mwake. Alishika nafasi ya nne katika michuano hiyo, lakini akapata umaarufu miongoni mwa waandamanaji wa Iran. Watu wengi walimsalimia katika uwanja wa ndege wa Tehran aliporejea nyumbani, na alisifiwa kwenye mitandao ya kijamii.

Chapisho kwenye ukurasa wake wa Instagram baadaye lilisema hijabu yake ilianguka "bila kukusudia" na aliomba msamaha kwa watu wa Iran katika mahojiano ya Televisheni ya Taifa kwa "mkanganyiko na wasiwasi". Hata hivyo, chanzo kimoja kimeiambia BBC kuwa mahojiano yake yalikuwa ya kulazimishwa.

Yulimar Rojas

Yulimar Rojas, Venezuela

Mwanamichezo

Mshindi wa medali ya Olimpiki (dhahabu na fedha) na bingwa mara tatu wa dunia, Yulimar Rojas alikuwa anashikilia rekodi ya dunia katika kuruka mara tatu kwa wanawake aliporekodi mita 15.74 katika Mashindano ya Ndani ya Riadha ya Dunia mnamo Machi. Sasa ameweka malengo yake juu ya mafanikio makubwa zaidi, akiruka m16.

Mzaliwa wa Caracas, Venezuela, na kukulia katika eneo maskini kwenye pwani ya Caribbean, amesifu mwanzo wake wa chini kabisa kwa kumsaidia kufanikiwa. Kwa sasa ni sehemu ya timu ya riadha ya Barcelona FC, Rojas amepata hadhi ya shujaa nchini mwake. Yeye anajihusisha na mapenzi ya jinsia moja na mtetezi wa sauti wa masuala ya LGBTQ.

Sisi wanawake hatupaswi kutishwa. Hakuna jambo lisilowezekana kwetu, tayari ni wazi kwamba tunaweza kudharauliwa lakini tayari tumeonesha kwa fahari kubwa kile tunachoweza.

Yulimar Rojas

Sally Scales

Sally Scales, Australia

Msanii

Mnamo 2022, mshauri wa sanaa Sally Scales aliteuliwa katika kikundi kinachofanya kazi na serikali ya Australia kabla ya kura ya maoni inayojulikana kama 'Sauti kwa Bunge' - mashauriano ya kihistoria ambayo, ikiwa yatafanikiwa, yatashuhudia wazawa wakiwakilishwa kabisa katika michakato ya bunge.

Kiongozi wa kitamaduni anayeheshimika na msanii, Mizani ni mwanamke wa Pitjantjatjara kutoka Pipalyatjara magharibi mwa ardhi ya Anangu Pitjantjatjara Yankunytjatjara (APY), katika maeneo ya mbali ya Australia Kusini. Yeye ni mwanamke wa pili kushikilia nafasi ya mwenyekiti wa kituo cha APY, na ni msemaji wa APY Art Centre Collective, kikundi cha makampuni ya kitamaduni yanayomilikiwa na wazawa.

Julia Gillard

Aliteuliwa na mshindi wa tuzo ya wanawake 100 mwaka 2018, mwanasiasa wa zamani Julia Gillard

"Sally ni muundaji wa sanaa nzuri na uelewa wa binadamu. Kwa kuwapa nuru na kuwashawishi wengine, anachochea mabadiliko mengi yanayohitajika ili kukomesha mchanganyiko mbaya wa ubaguzi wa rangi na ubaguzi wa kijinsia."

Nana Darkoa Sekyiamah

Nana Darkoa Sekyiamah, Ghana

Mwandishi

Kitabu chake the Sex Lives of African Women kimeelezewa kama "ripoti ya kushangaza juu ya jitihada za ukombozi wa kijinsia", katika tathmini ya kutisha ya Wachapishaji Kila Wiki. Iliorodheshwa na The Economist kama moja ya vitabu bora vya mwaka, ikionesha sauti mbalimbali kutoka bara zima na ughaibuni.

Mwandishi na mwanaharakati wa masuala ya wanawake, Nana Darkoa Sekyiamah pia ni mwanzilishi mwenza wa Adventures kutoka vyumba vya kulala vya Wanawake wa Afrika tovuti, podcast na tamasha ambalo linaunda maudhui ya kusimulia uzoefu wa wanawake wa Kiafrika kuhusu ngono na raha.

Wanaharakati wa wanawake wamefanikiwa kutengeneza nafasi kwa wanawake wote kujisimamia wenyewe. Lakini tunakabiliwa na upinzani, ambao ni matokeo ya mafanikio yetu na upinzani huu hasa unaathiri watu tofauti wa kijinsia na wasio na jinsia.

Nana Darkoa Sekyiamah

Geetanjali Shree

Geetanjali Shree, India

Mwandishi wa vitabu

Mtunzi wa riwaya na mwandishi Geetanjali Shree aliweka historia mwaka huu alipokuwa mwandishi wa kwanza wa Kihindi kushinda Tuzo ya Kimataifa ya Booker Prize kwa kitabu chake vha Tomb of the Sand, tafsiri ya Kiingereza ya riwaya yake Ret Samadhi. Tafsiri ya Kifaransa ya kitabu hicho pia iliorodheshwa kwa Tuzo ya Emile Guimet.

Shree huandika tamthiliya kwa Kihindi na isiyo ya kufikirika kwa Kihindi na Kiingereza. Ikiwa imegubikwa na matumizi ya ubunifu wa lugha na muundo, kazi zake zimetafsiriwa katika lugha nyingi za Kihindi na kigeni. Pia anafanya kazi kwenye maandishi ya maonesho kwa kushirikiana na kikundi cha michezo Vivadi, ambacho yeye ni mwanachama mwanzilishi.

Wanawake daima wamekuwa wakijadiliana kuhusu nafasi zao. Lakini katika siku zetu kumekuwa na maendeleo ya kuacha alama kwao katika nyanja zote za maisha, hata kama bila usawa katika tamaduni na matabaka.

Geetanjali Shree

Alexandra Skochilenko

Alexandra Skochilenko, Urusi

Msanii

Msanii wa St Petersburg Alexandra Skochilenko alikamatwa kwa kubadilisha vitambulisho vya bei ya maduka makubwa na ujumbe kuhusu vita nchini Ukraine, ikiwa ni pamoja na taarifa juu ya uwezekano wa idadi ya majeruhi katika shambulio la anga la ukumbi wa michezo wa Mariupol lililofanywa na vikosi vya Urusi. Baada ya kuripotiwa na mfanyabiashara mwingine, alishtakiwa chini ya sheria inayopiga marufuku 'upotoshaji' kuhusu majeshi ya Urusi.

Hivi sasa katika kituo cha kabla ya kesi akisubiri hukumu, anajiona kama mfungwa wa dhamiri na anakabiliwa na kifungo cha hadi miaka 10 gerezani.

Skochilenko ameandika vitabu vya vichekesho vinavyoangazia afya ya akili, ikiwa ni pamoja na Vidokezo juu ya msongo wa mawazo na Mania ni nini? Mpenzi wake ameripoti wasiwasi kuhusu afya ya Skochilenko akiwa kizuizini.

Velia Vidal

Velia Vidal, Colombia

Mwandishi

Msimulizi wa hadithi na mhamasishaji wa utamaduni kutoka mkoa wa El Chocó nchini Colombia, Velia Vidal ni mpenzi wa usomaji wa pamoja. Yeye ndiye mwanzilishi wa Motete, shirika linalokuza usomaji , pamoja na utamaduni wa kipekee wa Chocó. Pia anaandaa tamasha la kusoma na kuandika Chocó, akiona fasihi kama chombo cha kupambana na ukosefu wa usawa na ubaguzi wa rangi katika moja ya mikoa iliyotengwa zaidi Colombia.

Kitabu chake cha hivi karibuni, Aguas de Estuario, kilikuwa mshindi wa kwanza wa ruzuku ya uchapishaji kwa waandishi wa Afro-Colombia kutoka Wizara ya Utamaduni ya Colombia. Yeye ni mtafiti wa mradi wa Afluentes, mpango wa pamoja na Makumbusho ya Uingereza.

Sasa tunafahamu zaidi ukandamizaji wa kihistoria wa wanawake na haja ya kuurekebisha, lakini tunashindwa kutambua jinsi ubaguzi wa rangi unavyozidisha ukandamizaji huu kwa jamii ya Afro na watu wa asili.

Velia Vidal

Esraa Warda

Esraa Warda, Algeria/Marekani

Mcheza muziki wa asili

Mtoto wa wazazi waishio nje wenye asili ya Algeria, Esraa Warda ni shujaa wa kitamaduni ambaye amechukua ngoma ya jadi ya Algeria kutoka sebuleni hadi darasani. Anatetea uhifadhi wa mila za densi zinazoongozwa na wanawake wa Afrika Kaskazini, kwa kuzingatia hasa raï, namna inayohusishwa kihistoria na maandamano ya kijamii.

Yeye ni mwanafunzi wa Cheikha Rabia, mmoja wa wachache wa kike wa raï ya jadi huko ughaibuni. Warda ni msanii wa kutembelea na mwalimu na maonesho yake na warsha zimefanya wao kutembea duniani kote, kutoka Washington DC hadi London.

Uanaharakati na Utetezi

Lina Abu Akleh

Lina Abu Akleh, Mamlaka ya Palestina

Mwanaharakati wa haki za binadamu

Mtetezi wa haki za binadamu wa Palestina na Armenia Lina Abu Akleh ni mpwa wa mwandishi wa habari wa Palestina na Marekani Shireen Abu Akleh, mwandishi wa Al Jazeera ambaye aliuawa mwezi Mei wakati akiripoti uvamizi wa vikosi vya Israel katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu. Jeshi la Israel limesema kuna "uwezekano mkubwa" mmoja wa wanajeshi wake alimuua "kimakosa".

Lina sasa amekuwa sura ya kampeni ya haki na uwajibikaji kwa mauaji ya shangazi yake. Ana shahada ya uzamili katika masomo ya kimataifa yanayoangazia haki za binadamu. Alitajwa kama mmoja wa viongozi 100 wanaochipukia mwaka 2022 na TIME kwa utetezi wake.

Tunahitaji kuendeleza mahali ambapo shangazi yangu Shireen Abu Akleh aliachia na kuendelea kukuza mitazamo ya wanawake ili tuweze kuhakikisha kuwa hadithi tunazosimulia na habari tunazokusanya zina usawa, zilizokamilika na sahihi..bila wanawake hilo haliwezekani.

Lina Abu Akleh

Velmariri Bambari

Velmariri Bambari, Indonesia

Mwanaharakati

Akifanya kazi katika eneo la mbali la Indonesia, Velmariri Bambari amekuwa akipigania waathiriwa wa unyanyasaji wa kijinsia huko Sulawesi ya Kati. Amewashawishi wajumbe wa baraza la madiwani kuvunja sheria za kimila na kutowatoza faini manusura wa unyanyasaji wa kijinsia.

Katika sheria za kimila, adhabu ya "kusafisha kijiji" inabainisha kuwa wahusika wanaodhaniwa kuchafua maadili ya jadi wanapaswa kulipa faini. Sheria hii pia inatumika kwa waathirika. Kwa sababu ya kampeni zake, Bambari mara nyingi ndiye mtu wa kwanza kuwasiliana na polisi wakati unyanyasaji wa kijinsia unaporipotiwa. Ameshughulikia kesi kadhaa mwaka huu.

Ingawa mimi ni mlemavu wa viungo nataka kujitolea nguvu zangu kuwawezesha wanawake katika mazingira yangu kwa kutengeneza fursa zinazowawezesha kuwa na uhuru wa kifedha.

Velmariri Bambari

Tarana Burke

Tarana Burke, Marekani

Mwanaharakati

Hashtag hiyo ya #MeToo ilisambaa miaka mitano iliyopita, wakati mamilioni ya watu ulimwenguni kote waliposhiriki uzoefu wao wa unyanyasaji wa kijinsia. Lakini vuguvugu hilo lilianzishwa na manusura na mwanaharakati Tarana Burke mwaka 2006. Alibuni maneno hayo ili kuongeza uelewa wa unyanyasaji na unyanyasaji dhidi ya wanawake.

Wakati ujumbe wa Twitter wa mwaka 2017 wa mwigizaji Alyssa Milano ulipoongeza #MeToo, ulizua gumzo ulimwenguni kuhusu jinsi wanawake wanavyotendewa, na kuwapa manusura sauti yenye nguvu. Burke anaendelea kujitolea kutetea manusura wa unyanyasaji wakati anaendelea kupigania mabadiliko ya kitamaduni na kimuundo.

Sanjida Islam Choya

Sanjida Islam Choya, Bangladesh

Mwanafunzi

Bangladesh ina moja ya viwango vya juu vya ndoa za utotoni duniani, lakini Sanjida Islam Choya anajaribu kubadilisha hilo. Mama yake mwenyewe aliolewa akiwa na umri mdogo, lakini baada ya Choya kuhamasishwa na uwasilishaji wa shule kuhusu madhara ya ndoa za utotoni, aliamua kuchukua hatua.

Yeye na marafiki zake, walimu na washirika wake wanajiita Ghashforing (Grasshoppers) na kuripoti matukio ya ndoa za utotoni kwa polisi. Sasa katika chuo kikuu, kazi ya Choya na Ghashforing haijakoma na anawashauri wanachama wapya wa kikundi hicho. Kufikia sasa wanaripotiwa kuzuia ndoa za utotoni 50.

Heidi Crowter

Heidi Crowter, Uingereza

Mwanaharakati wa wenye ulemavu

Heidi Crowter amefanya kampeni ya kubadilisha mtazamo wa watu wenye hali ya Down Syndrome. Aliipeleka serikali ya Uingereza mahakamani kuhusiana na sheria inayoruhusu mimba ya vichanga vyenye Down Syndrome kutolewa, akisema ni ubaguzi. Mahakama Kuu ilitoa uamuzi dhidi ya pingamizi lake na kusema sheria hiyo inalenga kuweka uwiano kati ya haki za mtoto ambaye hajazaliwa na za wanawake. Mnamo Novemba, Crowter alipoteza rufaa yake, lakini alisema yeye na timu yake wanapanga "kuendelea kupigana" na kupeleka kesi hiyo katika Mahakama ya Juu.

Yeye ni kiongozi wa taasisi ya Positive About Down na afisa mwanzilishi wa Kikundi cha Sera ya Taifa ya Down Syndrome. Kitabu chake, I'm Just Heidi, kilichapishwa mwezi Agosti.

Nataka wanawake wajawazito wawe na taarifa sahihi kuhusu Down syndrome. Nataka watu waendelee na kutuona sisi kwa namna tulivyo!

Heidi Crowter

Sandya Eknaligoda

Sandya Eknaligoda, Sri Lanka

Mwanaharakati wa haki za binadamu

Mwanaharakati wa haki za binadamu, Sandya Eknaligoda anawasaidia maelfu ya kina mama na wake waliopoteza wapendwa wao wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Sri Lanka. Mumewe, Prageeth Eknaligoda, mwandishi mashuhuri wa habari za uchunguzi na mchora vibonzo, alitoweka Januari 2010. Alikuwa mkosoaji mkubwa wa serikali na alichunguza madai ya unyanyasaji dhidi ya waasi wa Tamil Tiger.

Tangu kutoweka kwake, mama huyo wa watoto wawili amekuwa akitafuta haki. Anawashutumu wafuasi wa Mahinda Rajapaksa, rais wa zamani wa Sri Lanka, kwa kuhusika na utekaji nyara wa mumewe. Wakati watuhumiwa wakitambuliwa, wote wameachiwa huru.

Mimi ni mwanamke ninayepigana kwa niaba ya wengine katika kila fursa, hujihusisha na mapambano na kushinda changamoto katikati ya matusi na kashfa, kupitia kujitolea.

Sandya Eknaligoda

Gohar Eshghi

Gohar Eshghi, Iran

Mwanaharakati wa kiraia

Gohar Eshghi amekuwa ishara ya uvumilivu na kuendelea nchini Iran. Mwanawe, Sattar Beheshti, alikuwa mwanablogu aliyefariki akiwa kizuizini muongo mmoja uliopita na Eshghi amekuwa akitoa wito wa haki tangu wakati huo, akishutumu mamlaka ya Iran kwa mateso na mauaji.

Yeye ni mmoja wa akina mama walalamikaji wa Iran, kundi linalotafuta haki kwa mauaji ya watoto wao. Akimshikilia Ayatollah Ali Khamenei, Kiongozi Mkuu wa Iran, akimhusisha na kifo cha mwanawe, alikuwa mmoja wa watia saini wa barua mnamo 2019, akitaka ajiuzulu. Wakati wa maandamano ya mwaka huu, kufuatia kifo cha Mahsa Amini, Eshghi aliondoa hijabu yake kwa mshikamano na waandamanaji.

Ceci Flores

Ceci Flores, Mexico

Mwanaharakati

Wanaume wenye silaha walimchukua mtoto wa Ceci Flores mwenye umri wa miaka 21 Alejandro mwaka 2015. Miaka minne baadaye, mwanawe mwingine, Marco Antonio, 31, alitekwa nyara na kundi la wahalifu. Flores anasema uanaharakati wake unasababishwa na hofu ya kufa bila kujua kilichotokea kwa watoto wake, waathiriwa wa kutoweka kwa lazima nchini Mexico.

Mwaka huu, nchi hiyo ilipiga hatua kubwa, ambapo watu 100,000 sasa wameorodheshwa kutoweka katika kile Ambacho Umoja wa Mataifa umekiita "janga la idadi kubwa". Chini ya uongozi wa Flores, mkusanyiko wa Madres Buscadoras de Sonora (Sonora's Searching Mothers) umesaidia kuwapata zaidi ya watu 1,000 waliopotea katika makaburi ya siri.

Geraldina Guerra Garcés

Geraldina Guerra Garcés, Ecuador

Mwanaharakati dhidi ya mauaji ya wanawake

Mtetezi wa haki za wanawake kwa zaidi ya miaka 17, Geraldina Guerra Garcés anafanya kazi kulinda waathiriwa wa unyanyasaji nchini Ecuador. Yeye ni mtaalamu wa kukusanya habari ili kuongeza kufichua mauaji ya wanawake kwa sababu ya jinsia yao.

Ni sehemu ya mpango wa Cartographies of Memory ambao unatafuta kuunda "ramani za maisha" za waathirika wa mauaji ya wanawake, kuweka kumbukumbu zao hai ili kusaidia kuchochea mabadiliko ya kitamaduni katika mitazamo. Guerra anafuatilia kesi za Muungano wa Wanawake na Mtandao wa Amerika Kusini Dhidi ya Unyanyasaji wa Kijinsia. Pia anawakilisha Wakfu wa Aldea na mtandao wa makazi ya wanawake.

Ikiwa hakutakuwa na hatua kali za kuzuia mauaji dhidi ya wanawake, hakutakuwa na maendeleo kwa mtu yeyote. Licha ya sheria mpya kuanza kutumika, bado tunauawa, na hilo lazima libadilike.

Geraldina Guerra Garcés

Moud Goba

Moud Goba, Uingereza

Mwanaharakati wa watu wa mapenzi ya jinsia moja

Kama mkimbizi mwenyewe, Moud Goba amefanya kazi kwa karibu miongo miwili na mashirika ya mashinani ambayo yanakuza ujumuishaji wa wakimbizi. Kwa sasa ni meneja wa kitaifa wa Micro Rainbow, ambayo hutoa makazi salama kwa wanaotafuta hifadhi ya LGBTQ + na wakimbizi. Anaongoza mradi wao wa nyumba, ambao hutoa vitanda 25,000 kwa mwaka kwa wasio na makazi, na pia anahusika katika mpango wao wa kuajiriwa.

Hivi karibuni Goba amesimamia mchakato wa ujumuishaji wa watu wa LGBTQ + waliowasili Uingereza kutoka Afghanistan. Yeye ni mmoja wa wanachama waanzilishi wa Uingereza Black Pride na mwenyekiti wa sasa wa bodi yao ya wadhamini.

Gehad Hamdy

Gehad Hamdy, Misri

Dakrari wa meno na kibinadamu

Daktari wa meno Gehad Hamdy pia ni mwanzilishi na meneja wa Speak Up, mpango wa Misri unaotumia jukwaa lake la mitandao ya kijamii kuangazia wahusika wa unyanyasaji wa kijinsia na unyanyasaji. Kumekuwa na mfululizo wa uhalifu dhidi ya wanawake kote nchini Misri mnamo 2022, na kufanya kuangaziwa kwa suala hilo.

Shirika hilo linawahimiza wanawake kuzungumzia unyanyasaji, huku pia likitoa msaada wa kisheria na kihisia na kuweka shinikizo kwa mamlaka kuchukua hatua. Kampeni ya Hamdy imetambuliwa mara kadhaa, ikiwa ni pamoja na kushinda tuzo ya haki sawa na kutobaguliwa katika Kongamano la Haki Duniani 2022.

Kuna safari ndefu; Hatuko popote karibu na mwisho. Kwa kweli, hatujaanza.

Gehad Hamdy

Judith Heumann

Judith Heumann, Marekani

Mtetezi wa haki za walemavu

Judith Heumann amejitolea maisha yake kupigania haki za watu wenye ulemavu. Baada ya kuugua polio akiwa mtoto, alikuwa mtumiaji wa kwanza wa kiti cha magurudumu kufanya kazi kama mwalimu huko New York City.

Yeye ni kiongozi anayetambuliwa kimataifa wa harakati za haki za walemavu, na uanaharakati wake ikiwa ni pamoja na kuhusika kwake kwa muda mrefu kumemfanya kuwa na jukumu kubwa katika utekelezaji wa sheria kuu. Heumann alihudumu katika tawala zote mbili za Clinton na Obama, na ana uzoefu wa miaka 20 usio wa faida.

Aliteuliwa na mshindi wa tuzo ya wanawake 100 mwaka 2020, mwanaharakati wa ulemavu Shani Dhanda

"Nimehamasishwa kweli na Judith, ambaye kwa zaidi ya miaka 30, amejitahidi kuendeleza haki za binadamu za watu wenye ulemavu duniani. Anabaki kuwa mtetezi asiyechoka na amekuwa sehemu ya nyakati muhimu katika harakati za haki za walemavu."

Jebina Yasmin Islam

Jebina Yasmin Islam, Uingereza

Mwanaharakati

Dada wa mwalimu wa shule ya msingi Sabina Nessa, ambaye aliuawa katika bustani ya London mnamo Septemba 2021, Jebina Yasmin Islam amekuwa mtetezi mkubwa wa usalama wa barabarani wa wanawake nchini Uingereza. Amefanya kampeni ya mabadiliko ya sheria, hivyo washtakiwa wanatakiwa kufika mahakamani kwa ajili ya hukumu.

Baada ya mauaji ya dada yake, Islam alikosoa ukosefu wa msaada wa serikali ya Uingereza, akisema unaashiria jinsi umuhimu mdogo ulivyowekwa katika ghasia za wanaume. Pia alizungumzia kuhusu ubaguzi wa rangi - wangepata matibabu bora, alisema, ikiwa familia yao ingekuwa "familia ya kawaida ya wazungu wa Uingereza". Islam anamuelezea dada yake kama "mfano wa kuigwa" ambaye alikuwa "mwenye nguvu, asiyeogopa, na mkali".

"Jipende kuliko mtu yeyote duniani."

Sabina Nessa

Ujumbe kutoka kwa jarida la Sabina Nessa, uliosambazwa na dada yake Jebina

Layli

Layli, Iran

Muandamanaji

Moja ya picha za kipekee za maandamano ya sasa nchini Iran ilikuwa ya msichana, aliyerekodiwa kutoka nyuma, akizibana nywele zake kwenye purukushani, na kujiandaa kuendelea kuandamana mitaani. Picha yake ikawa ishara ya ushujaa wa waandamanaji, lakini utambulisho wake ulikosewa kwa Hadis Najafi, mwanamke mwenye umri wa miaka 22 aliyeuawa wakati wa maandamano yanayoendelea.

Akizungumza na BBC Idhaa ya Kiajemi, Layli (sio jina lake halisi) alisema "atapigania watu kama Hadis Najafi na Mahsa Amini". Utawala wa Iran, alisema, "usitutishe na tishio la kifo. Tuna matumaini ya uhuru wa Iran."

Hadizatou Mani

Hadizatou Mani, Niger

Mwanaharakati wa kupinga utumwa

Aliuzwa na kuwa 'mke wa tano' akiwa na umri wa miaka 12, Hadizatou Mani alikuwa mtumwa chini ya desturi za wahaya, ambazo zinahusisha mwanaume mwenye ushawishi mkubwa kuchukua mke asiye rasmi kuwahudumia wake zake wanne halali. Baada ya kuachiliwa huru kisheria mwaka 2005, Mani aliolewa tena, lakini bwana wake wa zamani alimtuhumu kwa kuolewa tena wakati ana mume na kumshtaki. Alipatikana na hatia na kuhukumiwa kifungo cha miezi sita jela.

Mani alipinga uamuzi huo na Mahakama Kuu ya Niger ilibatilisha hukumu yake mnamo 2019, na kupiga marufuku desturi za wahaya kwa sababu hiyo. Kwa sasa ni mtetezi wa kupinga utumwa na anatumia jukwaa lake kuwasaidia wanawake wengine kutoroka.

Oleksandra Matviichuk

Oleksandra Matviichuk, Ukraine

Mwanasheria wa haki za binadamu

Kwa miaka 15, Oleksandra Matviichuk ameongoza Kituo cha Uhuru wa Raia (CCL), ambacho kwa pamoja kilitunukiwa Tuzo ya Amani ya Nobel ya 2022 kwa kazi yake ya kuorodhesha uhalifu wa kivita wa Urusi baada ya uvamizi wa Ukraine.

CCL inabeba urithi wa wapinzani wa Ukraine wa miaka ya 1960, ikizingatia haki za binadamu. Mwaka 2014, Kituo hicho kilikuwa shirika la kwanza la haki za binadamu kwenda Crimea, Luhansk, na Donetsk kuandika uhalifu wa kivita. Sasa wanatoa wito kwa mahakama ya kimataifa kuchunguza Urusi kwa madai ya ukiukaji wa haki za binadamu uliofanywa huko Chechnya, Moldova, Georgia, Syria, Mali, na Ukraine.

Oleksandra Matviichuk

Narges Mohammadi

Narges Mohammadi, Iran

Mwanaharakati wa haki za binadamu

Mwandishi wa habari na mteule wa Tuzo ya Amani ya Nobel Narges Mohammadi ni makamu wa rais wa Kituo cha Watetezi wa Haki za Binadamu nchini Iran na bila kuchoka amefanya kampeni ya kukomesha adhabu ya kifo. Wakati wa maandamano ya hivi karibuni nchini Iran, alituma barua kutoka gereza la Evin, akiutaka Umoja wa Mataifa kuizuia serikali ya Iran kutoa adhabu ya kifo kwa waandamanaji.

Mwaka 2010 Mohammadi alihukumiwa kifungo cha miaka 11 jela baadaye ikaongezeka hadi miaka 16 baada ya kutoa hotuba, akiwa kwa dhamana, akikosoa jinsi wafungwa walivyotendewa Evin. Makala yake ya White Torture inachunguza kifungo cha faragha, kulingana na mahojiano na wafungwa 16 wa zamani. Watoto wake wawili wanaishi uhamishoni na mumewe, mwanaharakati wa kisiasa Taghi Rahmani.

Tamana Zaryab Paryani

Tamana Zaryab Paryani, Afghanistan

Mwanaharakati

Siku chache baada ya kushiriki maandamano ya mwezi Januari ya kutaka haki ya kupata elimu na kazi, Tamana Zaryab Paryani na dada zake walionekana wakichukuliwa kwa nguvu kutoka nyumbani kwao na watu wenye silaha huku kukiwa na shutuma za kimataifa na wito wa kuachiliwa kwao, Taliban imekanusha kuhusika.

Alifanikiwa kupiga picha za majibu yake kuhusu kukamatwa kwake na kuiweka mtandaoni. Video iliyosambaa ya Paryani ilileta tahadhari kwa wanaharakati ambao walikuwa wakitoweka. Alikaa mahabusu kwa wiki tatu kabla ya kuachiliwa huru. Kwa sasa anaishi Ujerumani na kwa mshikamano na wanawake wa Iran, alichoma hijabu yake, hatua ambayo wanawake wengi wa Afghanistan waliiona ya utata.

Wakati wanawake duniani wanaendelea, wanawake wa Afghanistan wamerudishwa nyuma miaka 20. Miaka 20 ya mafanikio ya wanawake yameondolewa.

Tamana Zaryab Paryani

Alice Pataxó

Alice Pataxó, Brazil

Mwanaharakati wa kiasili

Mwanaharakati wa hali ya hewa, mwandishi wa habari na mshawishi, Alice Pataxó analenga kuhamasisha kuhusu jinsi sera za hivi karibuni za serikali ya Brazil za mazingira na kilimo zinavyotishia haki za ardhi za asili. Kama sauti kwa watu wa Pataxó, anataka kupinga maoni ya kikoloni kuhusu jamii za wenyeji na kutoa mwanga kuhusu mauaji ya wanaharakati wa mazingira.

Yeye ni mwandishi wa habari wa Colabora na anaunda maudhui kwa chaneli yake ya YouTube Nuhé, neno linalomaanisha ustahimilivu wa watu wa asili nchini Brazil.

Malala Yousafzai

Aliteuliwa na mshindi wa 2021, mwanaharakati wa elimu Malala Yousafzai

"Ninajivunia sana kumteua Alice Pataxó katika orodha ya wanawake 100 ya BBC mwaka huu. Kujitolea kwa Alice bila kutetereka kupigania hatua za hali ya hewa, usawa wa kijinsia, na haki za asili zinanipa matumaini kwamba ulimwengu endelevu na sawa zaidi unafikiwa."

Roya Piraei

Roya Piraei, Iran

Mwanaharakati

Mnamo Septemba, picha ya Roya Piraei ilisambaa. Mama yake, Minoo Majidi mwenye umri wa miaka 62, alikuwa akiandamana huko Kermanshah, mji mkubwa zaidi unaozungumza Kikurdi nchini Iran, alipopigwa risasi na kuuawa na vikosi vya usalama. Piraei alisimama kwenye kaburi la mama yake huku kichwa chake kikiwa kimenyolewa nywele, akiwa ameshika nywele zake zilizokatwa mikononi mwake na kutazama kamera kwa ukaidi.

Amekuwa miongoni mwa sura zilizogonga vichwa vya habari kimataifa baada ya maandamano ya kuipinga serikali kusambaa nchini Iran, kufuatia kifo cha Mahsa Amini, mwanamke wa Kikurdi mwenye umri wa miaka 22. Piraei tangu wakati huo amekutana na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron kupata uungwaji mkono wa kimataifa kwa maandamano yanayoendelea.

Yuliia Sachuk

Yuliia Sachuk, Ukraine

Kiongozi wa wenye ulemavu

Mtetezi wa haki za binadamu wa Ukraine Yuliia Sachuk ni mkuu wa Shirika la Fight for Right,linaloongozwa na wanawake wenye ulemavu. Alianzisha jibu la dharura kwa uvamizi wa Urusi nchini Ukraine, akifanya kazi saa nzima kuratibu mipango ya uokoaji na mashirika ya kimataifa ili kuokoa maisha ya maelfu ya Waukraine wenye ulemavu.

Sachuk ana shauku ya kuwawezesha wasichana na wanawake wenye ulemavu kushiriki katika kufanya maamuzi. Anashiriki katika mpango wa Kiongozi wa Obama Foundation Ulaya, alikuwa mshindi wa Tuzo ya Kitaifa ya Haki za Binadamu 2020, na ni mgombea wa Ukraine kwenye Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Watu wenye Ulemavu.

Suvada Selimović

Suvada Selimović, Bosnia na Herzegovina

Mwanaharakati wa amani

Ni miaka 30 tangu vita vilipoharibu Bosnia na Herzegovina, na Suvada Selimović sasa anaishi katika kijiji ambacho alisaidia kujenga upya, pamoja na wanawake wengine waliokimbia makazi yao ambao walirudi nyumbani. Mjane na mama kwa watoto wadogo, Selimovic alianzisha Anima, shirika la uanaharakati wa amani na uwezeshaji wa wanawake.

Baada ya mabaki ya mumewe kupatikana katika kaburi la pamoja mwaka 2008, alitoa ushahidi katika mahakama ya uhalifu wa kivita na kuwahimiza wanawake wengine kufanya hivyo. Leo, Anima huandaa warsha kwa wanawake wanaokabiliana na kiwewe cha vita, na huweka fursa kwao kuuza bidhaa wanazotengeneza.

Efrat Tilma

Efrat Tilma, Israel

Anayejitolea

Kama mtu wa kwanza aliyebadili jinsia katika Polisi wa Israeli, mwanaharakati Efrat Tilma anajibu wito wa dharura na anafanya kazi ili kuboresha uhusiano kati ya vikosi vya polisi na jamii ya LGBTQ +. Tilma alitoroka Israel akiwa kijana na kuhamia Ulaya, baada ya kukataliwa na familia yake na kupitia unyanyasaji wa polisi. Alifanyiwa upasuaji wa kurekebisha jinsia mwaka 1969 huko Casablanca, wakati upasuaji huo ulipigwa marufuku kwa kiasi kikubwa barani Ulaya.

Aliendelea kuwa mhudumu wa ndege mjini Berlin na kufunga ndoa. Alirejea Israel mwaka 2005, baada ya talaka yake, na akaona ni mahali pazuri kwa watu wachache wa mapenzi ya jinsia moja, jambo ambalo lilimtia moyo kujitolea na polisi.

Zhou Xiaoxuan

Zhou Xiaoxuan, China

Mwanaharakati wa wanawake

Kama uso wa harakati ya MeToo ya China, kesi ya Zhou Xiaoxuan ilifuatiwa na wanawake nchini China na watazamaji ulimwenguni. Mnamo 2018, alimshtaki Zhu Jun, mtangazaji nyota katika kituo cha televisheni cha CCTV kinachomilikiwa na serikali, akimtuhumu kwa kumpapasa na kumbusu kwa nguvu wakati wa mafunzo ya 2014. Alikana mashtaka hayo na kumshtaki kwa kumkashifu.

Kesi yake ilitupiliwa mbali kwa kukosa ushahidi wa kutosha na mwaka huu rufaa yake ilikataliwa katika kile ambacho baadhi ya vyombo vya habari vya kigeni viliita pigo kwa vuguvugu la MeToo la China. Zhou Xiaoxuan sasa anaunga mkono wanawake ambao wamenyanyaswa kingono na anahusika katika kuangazia masuala ya wanawake nchini China.

Mwanamke anayekata nywele zake

Mwanamke anayekata nywele zake, Iran

Muandamanaji

Maandamano makubwa yalizuka nchini Iran mwaka huu, kufuatia kifo cha Mahsa Amini, mwanamke wa Kikurdi mwenye umri wa miaka 22 aliyekamatwa na polisi wa maadili mjini Tehran mnamo Septemba 13 kwa madai ya kukiuka sheria kali za Iran zinazowataka wanawake kufunika nywele zao kwa hijabu.

Mwaka huu tulitaka kutambua jukumu ambalo wanawake wametekeleza katika maandamano, kupigania uhuru wao na dhidi ya hijabu ya lazima.

Ukataji nywele umekuwa moja ya alama za vuguvugu ambalo limesambaa kwa watu mashuhuri, wanasiasa na wanaharakati kote duniani. Inaonekana na baadhi ya jamii nchini Iran kama ishara ya jadi ya maombolezo.

Afya & Sayansi

Aye Nyein Thu

Aye Nyein Thu, Myanmar

Daktari

Aye Nyein Thu ni mtu wa kujitolea mstari wa mbele katika maeneo yenye mgogoro nchini Myanmar, akiangazia jimbo la mbali na maskini la Chin. Alijenga hospitali ya muda na ukumbi mdogo wa upasuaji mnamo Novemba 2021 na tangu wakati huo amekuwa akitibu wagonjwa na majeruhi.

Katika muda wake wa ziada, anasafiri kwenda mikoa mingine ambako matibabu hayapatikani, kusaidia wagonjwa wa ndani ikiwa ni pamoja na watu waliokimbia makazi yao. Katika kipindi cha kazi yake, amekuwa na mashtaka ya 'kusababisha uchochezi wa ghasia' zilizoletwa dhidi yake na jeshi la Myanmar, ambalo lilimshutumu kwa kuunga mkono makundi ya wanamgambo wanaoipinga serikali yanayojulikana kama People's Defence Forces.

Sirisha Bandla

Sirisha Bandla, India

Mhandisi wa anga

Sirisha Bandla alikwenda pembezoni mwa anga za mbali kama sehemu ya ujumbe wa kihistoria wa 2021 Unity 22, chombo cha kwanza cha Virgin Galactic kilichokuwa kimetengenezwa kikamilifu - na kumfanya kuwa mwanamke wa pili raia wa India kwenda anga za mbali.

Akiendeleza mapenzi yake na masuala ya anga za mbali akiwa na umri mdogo, Bandla aliendelea na masomo ya uhandisi wa anga nchini Marekani. Sasa ni Makamu wa Rais wa Masuala ya Serikali na Shughuli za Utafiti wa Virgin Galactic, jukumu ambalo linajumuisha kufanya kazi na wateja wa utafiti,majaribio ya sayansi na teknolojia kwenye SpaceShip ya VG.

Sunny Leone

Aliteuliwa na mshindi wa 2016, mwigizaji Sunny Leone

"Katika tasnia inayotawaliwa na wanaume, kwa Sirisha kushinda kila kitu na kwa kuzingatia tu bidii yake na kujitolea kwake kunamfanya kuwa msukumo kwangu na, muhimu zaidi, kwa wasichana wote wadogo huko nje wenye ndoto sawa."

Victoria Baptiste

Victoria Baptiste, Marekani

Muuguzi na mwalimu wa chanjo

Muuguzi katika jimbo la Maryland nchini Marekani, Victoria Baptiste akiwaelimisha watu kuhusu chanjo. Anaelewa kwa nini jamii ya watu weusi inaweza kuwa na shaka juu ya hatua za matibabu: Baptiste ni uzao wa Henrietta Lacks, mwanamke mweusi ambaye alikufa kwa saratani ya shingo ya kizazi mnamo 1951 ambaye seli zake, zilizochukuliwa bila idhini yake, zilikuwa za kwanza kukuzwa katika maabara.

Zikijulikana kama seli za HeLa, zimekuwa zikitumika katika utafiti wa kimatibabu tangu wakati huo, lakini familia haikujua kwa miongo kadhaa. Sasa sehemu ya Henrietta Lacks Foundation, Baptiste pia ni Balozi wa Goodwill ya WHO ya kutokomeza saratani ya shingo ya kizazi.

Niloufar Bayani

Niloufar Bayani, Iran

Mwanaikolojia

Mhifadhi Niloufar Bayani alikuwa mmoja wa wanamazingira kadhaa waliokamatwa nchini Iran mwaka 2018 baada ya kutumia kamera kufuatilia spishi zilizo hatarini kutoweka. Walishtakiwa kwa kukusanya taarifa za siri kuhusu maeneo nyeti ya kimkakati, na Bayani alihukumiwa kifungo cha miaka kumi jela.

Bayani alikuwa mkuu wa programu ya Wakfu wa Urithi wa Wanyamapori wa Uajemi, uliojitolea kuokoa duma wa Asia (jamii ndogo ya duma walio katika hatari ya kutoweka na wanaishi nchini Iran pekee) na spishi nyingine. Katika waraka uliopatikana na BBC Persian, alisema Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran lilimfanyia "mateso makali zaidi ya kiakili, kihisia na kimwili na vitisho vya ngono kwa takribani saa 1,200". Mamlaka ya Iran imekanusha madai hayo.

Sandy Cabrera Arteaga

Sandy Cabrera Arteaga, Honduras

Mtetezi wa haki za masuala ya uzazi

Mwanafunzi wa falsafa, mwandishi na mwanaharakati, Sandy Cabrera Arteaga ni mtetezi wa haki za ngono na uzazi. Anatoa warsha kuhusu kidonge cha 'morning after' na ni msemaji wa 'Hablemos lo que es' (Tuzungumze kuhusu hali ilivyo) - kampeni ya elimu na jukwaa la kidigitali kuhusu uzazi wa mpango wa dharura.

Pia anafanya kazi kwenye taasisi ya Acción Joven iliyojikita kwa vijana kuhusu haki za binadamu, ngono na uzazi kwa vijana. Ana ufasaha katika lugha ya ishara ya Honduran na kama binti pekee wa mama ambaye ni kiziwi, anajivunia malezi yake jumuishi na ya kujali.

Samrawit Fikru

Samrawit Fikru, Ethiopia

Mjasiriamali wa teknolojia

Ingawa hakuwahi kutumia kompyuta hadi alipokuwa na umri wa miaka 17, mtayarishaji programu Samrawit Fikru ni mwanzilishi wa Hybrid Designs, moja ya kampuni zilizoanzisha programu ya teksi ya Ethiopia RIDE.

Uzoefu wake mwenyewe akihisi si salama kuchukua teksi baada ya kazi na kulazimika kuhangaika na madereva waliotaka kumtoza ziada kulimfanya atengeneze programu hiyo, ambayo alianza na chini ya $2,000 (karibu pauni 1,700). Kampuni yake iliendelea kuajiri wafanyakazi wengi. Kuna wanawake wachache katika sekta ya teknolojia nchini Ethiopia na Fikru anataka kuhamasisha kizazi kijacho cha wajasiriamali wadogo.

Biashara inayomilikiwa na wanawake inaongezeka kwa idadi; Sasa tunahitaji wasichana wadogo zaidi kupata fedha ili kufanikisha mawazo yao ya ubunifu.

Samrawit Fikru

Wegahta Gebreyohannes Abera

Wegahta Gebreyohannes Abera, Tigray, Ethiopia

Mfanyakazi wa misaada ya kibinadamu

Mfanyakazi wa misaada ya kibinadamu, Wegahta Gebreyohannes Abera pia ni mwanzilishi wa Hdrina, shirika lisilo la faida ambalo linalenga kutokomeza utapiamlo unaosababishwa na vita huko Tigray. Hdrina ina miradi kadhaa ya kusaidia wanawake na watoto walioathirika na vita, ikiwa ni pamoja na mpango wa dharura wa kulisha katika kambi ya wakimbizi wa ndani (IDP) na mradi wa bustani ya mijini.

Shirika hilo pia linaendesha mradi wa uwezeshaji wanawake kwa manusura wa unyanyasaji wa kijinsia unaohusiana na migogoro na wanawake ambao, kutokana na umaskini unaosababishwa na vita, wamegeuka kuwa wafanyabiashara wa ngono.

Dilek Gürsoy

Dilek Gürsoy, Ujerumani

Daktari wa upasuaji wa moyo

Mzaliwa wa Ujerumani na wazazi wahamiaji wa Uturuki, Dk Dilek Gürsoy ni daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mtaalamu wa moyo bandia. Alilifanya jarida la Forbes nchini Ujerumani, kumsifu kwa kuwa daktari wa kwanza wa upasuaji wa barani Ulaya kupandikiza moyo bandia.

Amekuwa mstari wa mbele katika utafiti wa moyo bandia kwa zaidi ya muongo mmoja, akishughulikia maendeleo ya njia mbadala ya upandikizaji wa moyo kutokana na viwango vya chini vya uchangiaji wa viungo, kwa kuzingatia anatomia ya kike. Ameandika tawasifu na sasa yuko katika mchakato wa kuanzisha kliniki yake ya moyo.

Sofía Heinonen

Sofía Heinonen, Argentina

Mhifadhi

Akiwa amejitolea kulinda viumbe hai, mwanabiolojia Sofía Heinonen aliongoza juhudi za kwanza za kubadilisha mgogoro wa kutoweka huko Amerika Kusini, na kubadilishwa tena kwa Esteros del Iberá, mfumo mkuu wa ikolojia ya ardhi oevu nchini Argentina na kubwa zaidi duniani. Ametumia zaidi ya miaka 30 kuchangia ujenzi wa maeneo yaliyohifadhiwa.

Chini ya uongozi wake, mradi wa Rewilding Argentina unafanya kazi katika ikolojia kuu nne, ikiwa ni pamoja na hatua ya Patagonia, chini ya mfano ambao unaangalia kugeuza ardhi ya binafsi kuwa mbuga za kitaifa zilizohifadhiwa na kurejesha spishi za asili ili kurejesha mifumo ya ikolojia na kujenga ecotourism endelevu.

Kimiko Hirata

Kimiko Hirata, Japan

Mwanaharakati wa tabia nchi

Mpinzani mkali wa nishati ya makaa ya mawe, Kimiko Hirata ametumia karibu nusu ya maisha yake kupigania kuiachisha Japan utegemezi wake kwa nishati ya visukuku - kwa kiasi kikubwa zaidi kuchangia mabadiliko ya tabia nchi. Kampeni yake ya vijijini ilisababisha kufutwa kwa mitambo 17 ya kuzalisha umeme wa makaa ya mawe. Ni mwanamke wa kwanza Mjapani kushinda Tuzo ya Mazingira ya Goldman.

Hirata aliacha kazi yake ya uchapishaji na kuwa mwanaharakati wa hali ya hewa katika miaka ya 1990 baada ya kusoma kitabu cha Al Gore cha Earth in the Balance. Sasa ni Mkurugenzi Mtendaji wa shirika huru la Climate Integrate, lililoanzishwa Januari 2022, ambalo linakabiliana na uharibifu.

Judy Kihumba

Judy Kihumba, Kenya

Mkalimani wa lugha ya ishara

Akiwa mtetezi wa afya ya akili ya uzazi na ustawi wa mama wauguzi viziwi, Judy Kihumba aliingilia kati kutoa taarifa za afya kwa wanawake wote alipogundua kuwa baadhi ya hospitali nchini Kenya hazikuwa na wakalimani wa lugha ya alama.

Yeye ndiye mwanzilishi wa taasisi ya Talking Hands, Listening Eyes on Postpartum Depression (THLEP) na husaidia wanawake wenye ulemavu wa kusikia katika safari ya uzazi. Kihumba alianzisha shirika hilo baada ya kupata msongo wa mawazo baada ya kujifungua mwenyewe mwaka 2019. Mwaka huu waliandaa kundi la kwanza la 'baby shower', ambalo liliwakutanisha akina mama viziwi 78 na watendaji wa afya na washauri.

Marie Christina Kolo

Marie Christina Kolo, Madagascar

Mjasiriamali wa hali ya hewa

Mjasiriamali wa kijamii wa kijani na ecofeminist, Marie Christina Kolo alikuwa sehemu ya ujumbe rasmi wa Madagascar kwa COP27. Anatetea haki za binadamu na masuala ya kijinsia ya mabadiliko ya tabianchi,wakati nchi yake inastahimili ukame mfululizo ambao unasababisha upatikanaji mgumu wa chakula kwa mamilioni ya watu. Umoja wa Mataifa umeitaja kuwa njaa ya kwanza duniani inayosababishwa na mabadiliko ya tabianchi.

Kolo ni mkurugenzi wa kanda wa shirika lisilo la kiserikali la People Power Inclusion, ambalo linalenga kupambana na umaskini kupitia uchumi wa kijani. Biashara yake ya kijamii, Green'N'Kool, ni jukwaa la kitaifa linaloongoza la haki ya hali ya hewa. Kama manusura wa unyanyasaji wa kijinsia, alianzisha vuguvugu la Women Break the Silence, ambalo linapambana dhidi ya utamaduni wa ubakaji.

Hatutaki kuonekana tu kama waathirika maskini wa athari za hali ya hewa, mfumo dume na vurugu. Ninajisikia matumaini na fahari sana ninapoona kwamba sisi wanawake tunaweza kuwa imara, licha ya matatizo yote.

Marie Christina Kolo

Iryna Kondratova

Iryna Kondratova, Ukraine

Daktari wa watoto

Licha ya kukabiliwa na mashambulizi makali ya makombora, Dkt Iryna Kondratova na timu yake waliendelea kuwahudumia bila kuchoka wanawake wajawazito, watoto wachanga na kina mama katika Kituo cha Perinatal cha Mkoa wa Kharkiv. Walianzisha wodi ya wafanyakazi katika chumba cha chini cha hospitali, na kuhatarisha maisha yao kukaa na watoto wenye uangalizi mkubwa ambao hawakuweza kuhamishwa, hata wakati ving'ora vya uvamizi wa anga vikisikika.

Akiwa mkuu wa kituo hicho, Dkt Kondratova alichukua instagram ya David Beckham mwezi Machi, kuangazia changamoto zinazowakabili. Timu yake imetoa msaada wa matibabu na kisaikolojia kwa zaidi ya wanawake 3,000 kutoka Luhansk na Donetsk tangu 2014.

Nyumba zetu, barabara, vituo vya umeme, hospitali na maisha vimeharibiwa. Lakini ndoto zetu, matumaini yetu na imani yetu ni hai na yenye nguvu kuliko hapo awali.

Iryna Kondratova

Asonele Kotu

Asonele Kotu, Afrika Kusini

Mjasiriamali wa teknolojia

Wazo la biashara yake lilizaliwa baada ya Asonele Kotu kutaka kipandikizi chake cha uzazi wa mpango kiondolewe, lakini hakuweza kupata mtu wa kumsaidia. Kisha alianzisha FemConnect, mwanzo ambao hutoa suluhisho la teknolojia ili kupunguza umaskini wa kipindi na kupunguza mimba za utotoni.

Jukwaa hilo linaruhusu watumiaji kupata tiba kwa masuala ya ngono na uzazi kwa njia ya teknolojia ya mawasiliano bila unyanyapaa au ubaguzi, pamoja na bidhaa za usafi wa njia za uzazi wa mpango na njia sawa na hiyo ya kuagiza chakula mtandaoni. Kotu ana shauku ya kutokomeza umaskini wa kipindi na kuboresha upatikanaji wa huduma bora za afya, hasa kwa vijana walio katika hatari na wale walio katika jamii zilizotengwa na zisizostahili.

Imekuwa vizuri kuangalia dhamira ya vijana kubuni suluhisho la matatizo, ili kuhakikisha kuwa kizazi kijacho hakipati mapambano kama hayo ambayo wazazi wetu waliyafanya

Asonele Kotu

Erika Liriano

Erika Liriano, Jamhuri ya Dominika

Mjasiriamali wa Kakao

Akilenga kurejelea mnyororo wa usambazaji wa kakao, Erika Liriano anaendesha mwanzo wa kugawana faida katika Jamhuri ya Dominika. Liriano alianzisha INARU na dada yake, Janett, kwa lengo la kufanya uzalishaji na usambazaji wa kakao kuwa wa haki na endelevu zaidi. Mwaka huu, kuanza kwao kulipata ufadhili wa mbegu.

Kihistoria, sekta ya kakao imekuwa ya unyonyaji kwa wakulima wadogo lakini kampuni yao inahakikisha utafutaji wa maadili na mshahara wa haki kwa wazalishaji wa Dominika. Wazaliwa wa New York, akina dada hao wanatoka katika familia ya wakulima na wajasiriamali katika Jamhuri ya Dominika. Sasa wanashirikiana na mashamba yanayoendeshwa na wanawake, vyama vya ushirika na wasambazaji kote nchini.

Nguvu ya kuamua njia yako mwenyewe ni kitu ambacho wanadamu wote wanapaswa kuwa na haki, na hiyo ni pamoja na nguvu ya mwanamke kuchagua ni aina gani ya maisha anayotaka mwenyewe.

Erika Liriano

Naja Lyberth

Naja Lyberth, Greenland

Mwanasaikolojia

Mtaalamu wa Naja Lyberth alikuwa na umri wa miaka 13 tu wakati alipowekewa kifaa cha intrauterine (IUD), kinachojulikana kama koili, kama sehemu ya kampeni ya kudhibiti uzazi iliyofanywa kwa Inuit Greenlanders na madaktari wa Denmark wakati wa miaka ya 1960 na 70. Mwaka huu Denmark na Greenland zilikubaliana rasmi kuanzisha uchunguzi kuhusu vitendo hivi, ambavyo huenda viliathiri karibu wanawake na wasichana 4,500.

Kampeni za Lyberth kusaidia wanawake hawa, ikiwa ni pamoja na wale wanaoshuku kuwa koili ndio sabababu ya changamoto yao ya masuala ya uzazi. Ameanzisha kikundi cha Facebook kwa wanawake kuungana na kusaidiana.

Wanawake zaidi na zaidi ambao ni manusura wanakuwa mfano wa kuigwa kwa wanawake wengine. Kuzungumza nje mara nyingi hufanya hofu kutoweka, unapogundua kuwa hutahukumiwa. Hatuwezi kudhibitiwa na hofu zetu.

Naja Lyberth

Nigar Marf

Nigar Marf, Iraq

Muuguzi

Kama muuguzi mkuu katika kitengo kikuu cha walioungua moto nchini Iraq Kurdistan, kazi ya Nigar Marf ni pamoja na kuwatibu wanawake ambao wamejichoma moto.Vitendo hivi bado ni vya kawaida miongoni mwa wasichana katika eneo hilo, kama njia ya maandamano.

Marf amefanya kazi katika hospitali kwa karibu miaka 25, katika majeraha ya kuungua kwa watoto na uangalizi mkubwa. Katika wodi yake pia anawahudumia wagonjwa ambao wamepata majeraha ya kuungua kwa ajali. Wanawake wengi anaowatibu walipitia unyanyasaji wa kiakili na kimwili kabla ya kuamua kujichoma moto; Baadhi yao walikuwa na umri wa miaka 16.

Monica Musonda

Monica Musonda, Zambia

Mfanyabiashara

Mwanasheria wa kampuni aliyegeuka kuwa mjasiriamali, Monica Musonda ndiye mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Java Foods, kampuni ya usindikaji wa chakula yenye makao yake nchini Zambia na mtengenezaji wa tambi za papo hapo katika ukanda wa kusini mwa Afrika. Maono yake ni kuzalisha bidhaa nafuu za chakula kwa kutumia fursa ya mavuno makubwa ya ngano ya Zambia, pamoja na mahitaji ya vyakula rahisi zaidi na kubadilisha mifumo ya matumizi.

Musonda, ambaye ni mtetezi wa lishe, anawashauri wajasiriamali wengine kadhaa na kuzungumzia masuala yanayoathiri wanawake katika biashara. Ameshinda tuzo nyingi, na ametambuliwa kwa kazi yake ya kuimarisha mifumo ya kilimo na chakula barani Afrika.

Ifeoma Ozoma

Ifeoma Ozoma, Marekani

Mtaalamu wa sera za umma na teknolojia

Baada ya kukiuka makubaliano yake ya kutotoa taarifa (NDA) kumshutumu mwajiri wake wa zamani Pinterest kwa ubaguzi wa kijinsia na rangi, Ifeoma Ozoma amedhamiria kuwasaidia wafanyakazi kupambana na vitendo viovu kazini. Akawa mdhamini mwenza wa Sheria ya Silenced No More, ambayo inaruhusu kila mfanyakazi huko California kushiriki habari kuhusu ubaguzi au unyanyasaji bila kujali kusaini NDA. Pinterest ilifanya ukaguzi mahali pa kazi kufuatia madai ya Ozoma na kusema inaunga mkono sheria hiyo.

Ozoma pia aliandika Kitabu cha Mfanyakazi wa Teknolojia, mkusanyiko wa rasilimali za kusaidia wafanyikazi kuzungumza, na kuanzisha Earthseed, ambayo inashauri mashirika juu ya usawa katika sekta ya teknolojia.

Yuliia Paievska

Yuliia Paievska, Ukraine

Mtaalamu wa afya

Mganga wa kiraia wa Ukraine aliyepambwa, na mwanzilishi wa taasisi ya Taira's Angels kitengo cha matibabu cha kujitolea kinachosifiwa kwa kuokoa mamia ya raia waliojeruhiwa na wanajeshi. Yuliia Paievska, anayejulikana zaidi kama Taira, alikamatwa na vikosi vya Urusi mwezi Machi wakati akisaidia kuwahamisha raia kutoka Mariupol.

Alikuwa akitumia kamera ya mwili kuandika kazi ya timu yake katika jiji lililozingirwa, na picha hizo zilitolewa kwa vyombo vya habari. Alipoachiliwa miezi mitatu baadaye, Paievska alizungumzia hali mbaya na ya kikatili aliyokumbana nayo wakati akiwa mateka, akielezea kuzuiliwa kwake kama "jehanamu".

Jane Rigby

Jane Rigby, Marekani

Mnajimu na mwanaastrofizikia

Mwanaastrofizikia wa Nasa Dk Jane Rigby anajifunza jinsi galaksi zinavyobadilika. Alikuwa mmoja wa wanasayansi muhimu katika timu ya kimataifa iliyozindua na kupeleka James Webb, darubini kubwa zaidi ya anga za juu duniani. Mnamo Julai, picha za kwanza za rangi kamili zilizochukuliwa na Webb zikawa mtazamo wa kina zaidi wa ulimwengu hadi sasa.

Rigby amechapisha zaidi ya karatasi 100 za kisayansi zilizopitiwa na ameshinda tuzo nyingi kwa utafiti wake. Yeye pia ni mtetezi wa usawa na ujumuishaji katika STEM (Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati).

Nilipokuwa mwanafunzi, sikuwa na ufahamu wa mfano wowote wa kuigwa wa LGBTQ. Natumai mimi ni sehemu ya kizazi cha mwisho ambacho kilikua bila mifano ya kuigwa ya kufuata.

Jane Rigby

Ainura Sagyn

Ainura Sagyn, Kyrgyzstan

Mhandisi

Kama mhandisi wa kompyuta, mwanaikolojia, na Ainura Sagyn amekuwa akitumia ujuzi wake kujenga ufumbuzi wa teknolojia kwa matatizo ya mazingira. Alianzisha Tazar, programu ambayo inaunganisha wazalishaji wa taka kila mtu kutoka kaya na watu binafsi hadi migahawa, viwanda na maeneo ya ujenzi na wachakataji. Programu hiyo inalenga kupunguza taka zinazopepea na kujaza ardhi na hatimaye kukabiliana na tatizo la uendelevu katika nchi za Asia ya Kati.

Pia ameongoza warsha katika coding na STEM (Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati) kwa zaidi ya wasichana wa shule 2,000 katika mikoa tofauti ya Kyrgyzstan.

Without women’s leadership and participation in climate responses today, it is unlikely that solutions for a sustainable planet and a gender-equal tomorrow will be realised.

Ainura Sagyn

Monica Simpson

Monica Simpson, Marekani

Mwanaharakati wa haki ya uzazi

Kama mkurugenzi mtendaji wa SisterSong, umoja wa wanawake wa rangi unaofanya kazi kwa haki ya uzazi katika majimbo ya kusini mwa Marekani, Monica Simpson analenga kupigania uhuru wa kijinsia na uzazi. Suala hilo lilirejea katika uangalizi mwaka huu baada ya Mahakama Kuu ya Marekani kubatilisha uamuzi wa Roe v Wade uliofanya uavyaji mimba kisheria kuwa haki kote nchini.

Simpson pia ni mwimbaji na msanii wa maneno anayezungumzwa, akichochea uanaharakati wake na sanaa yake. Yeye ni mtoa huduma ya saikolojia aliyethibitishwa na mjumbe mwanzilishi wa bodi ya Black Mamas Matter Alliance, akifanya kazi ya kuendeleza afya ya uzazi ya mwanamke mweusi.

Maryna Viazovska

Maryna Viazovska, Ukraine

Mwanahisabati

Mwanahisabati wa Ukraine ambaye mapema mwaka huu alikuwa mwanamke wa pili tu katika historia kushinda medali ya kifahari ya Fields - mara nyingi huelezewa kama Tuzo ya Nobel ya Hisabati na kutolewa kila baada ya miaka minne. Maryna Viazovska alishinda tuzo hiyo kwa kazi yake kwenye fumbo la miaka 400. Maryna huweza kufanya mambo ambayo si dhahiri kabisa ambayo watu wengi walijaribu na kushindwa kufanya.

Kulingana na Taasisi ya Teknolojia ya Shirikisho la Uswisi huko Lausanne (EPFL), Viazovska ni profesa na Mwenyekiti wa Nadharia ya Nambari katika Taasisi ya Hisabati.

Yana Zinkevych

Yana Zinkevych, Ukraine

Mwanasiasa na mtu wa kujitolea wa matibabu katika mstari wa mbele

Kuokoa maisha katika mstari wa mbele wa vita, Hospitali ni shirika la kujitolea la wahudumu wa afya. Wakiongozwa na Yana Zinkevych, wanafanya kazi ya kuwahamisha watu kutoka uwanja wa vita. Zinkevych alijitolea kwa matibabu baada ya kuacha shule, na alianzisha kikosi hicho mnamo 2014 mwanzoni mwa uhasama nchini Ukraine.

Yeye binafsi amewabeba wanajeshi 200 waliojeruhiwa kupelekwa kwenye eneo la usalama. Timu yake inaendelea kutoa huduma ya kwanza kwa wanajeshi na raia waliojeruhiwa, hufanya mafunzo ya matibabu, na imefanya uokoaji karibu 6,000. Kijana huyo mwenye umri wa miaka 27 pia ni mmoja wa wanachama wadogo zaidi wa bunge la Ukraine na ni mkuu wa kamati ndogo ya dawa za kijeshi.

Wanawake 100- BBC World Service

Wanawake 100 ni nini?

Wanawake 100 wa BBC huwataja wanawake 100 wenye ushawishi na msukumo kote duniani kila mwaka. Tunaunda makala, vipengele na mahojiano kuhusu maisha yao - hadithi ambazo zinawaweka wanawake katika nafasi ya kipekee.

Fuatilia BBC wanawake 100 kwenye Instagram, Facebook na Twitter. Jiunge na mazungumzo kwa kutumia #BBC100Women.

Wanawake 100 walichaguliwa vipi?

Timu ya Wanawake 100 ya BBC iliandaa orodha fupi kulingana na majina waliyokusanya na yale yaliyopendekezwa na mtandao wa BBC wa timu za Lugha za Huduma za Dunia, pamoja na BBC Media Action.Tulikuwa tunatafuta wagombea ambao walikuwa wamegonga vichwa vya habari au kushawishi hadithi muhimu katika kipindi cha miezi 12 iliyopita, pamoja na wale ambao wana hadithi za kuhamasisha kusimulia, au wamepata kitu muhimu au kushawishi jamii zao kwa njia ambazo hazingeweza kutoa habari.Majina yalitathiminiwa dhidi ya kaulimbiu ya mwaka huu - maendeleo ambayo yamefanywa katika maeneo tofauti katika muongo mmoja uliopita.

Tulichunguza mada ambazo ziligawanya maoni, kama vile haki za uzazi ambapo maendeleo ya mwanamke mmoja yanaweza kuwa majuto ya mwingine, na kuteua wanawake ambao wameleta mabadiliko yao wenyewe. Orodha hiyo pia ilipimwa kwa uwakilishi wa kikanda na kutopendelea upande wowote, kabla ya majina ya mwisho kuchaguliwa.

Baadhi ya wanawake katika orodha hiyo wanaonekana bila kujulikana au bila jina la ukoo ili kuwalinda wao na familia zao, kwa ridhaa yao na kufuata miongozo yote ya Sera ya Wahariri na Usalama wa BBC.